Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Siku zote za kiapo chake cha kujitenga, hatanyoa nywele zake. Mpaka muda wa kiapo chake cha kujitakasa kwa Yawe utakapomalizika, atakuwa mutakatifu, ataacha nywele zake zikuwe ndefu.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 6:5
9 Referans Kwoze  

Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”


hakuweza kuvumilia, akamufunulia siri yake, akisema: “Nywele zangu hazijapata kunyolewa hata kidogo. Mimi nimewekwa Munaziri wa Mungu tangu katika tumbo la mama yangu. Kama nikinyolewa nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”


kwa maana utabeba mimba na kuzaa mutoto mwanaume. Nywele za mutoto huyo zisinyolewe hata kidogo, maana atakuwa Munaziri wa Mungu tangu kuzaliwa kwake. Naye ataanza kuwakomboa Waisraeli toka katika mikono ya Wafilistini.”


Naye Delila akamufanya Samusoni alale usingizi juu ya magoti yake, akamwita mutu amunyoe ile misuko yake saba. Kisha Delila akaanza kumutesa Samusoni kwa sababu sasa nguvu zilikuwa zimemutoka.


Paulo akaendelea kule Korinto kwa muda wa siku nyingi. Kisha akaagana na wandugu waamini, akasafiri kwa njia ya chombo na kwenda katika inchi ya Suria. Nao Prisila na Akila walikuwa pamoja naye. Mbele ya kuondoka, Paulo alinyolewa kwenye kivuko cha Kenkurea, kwa maana alikuwa ametimiza kiapo alichofanya mbele ya Mungu.


Muda wote atakaokuwa munaziri asikule kitu chochote kinachotokana na muzabibu, tangu kokwa hata maganda yake.


Hawatanyoa vichwa vyao wala kuacha nywele zao zikuwe ndefu. Lakini watapunguza nywele zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite