Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Uwape Waisraeli maagizo haya: Ikiwa mwanaume au mwanamuke atafanya kiapo kuwa munaziri, ni kusema kujitenga kwa ajili ya Yawe,

Gade chapit la Kopi




Hesabu 6:2
21 Referans Kwoze  

kwa maana utabeba mimba na kuzaa mutoto mwanaume. Nywele za mutoto huyo zisinyolewe hata kidogo, maana atakuwa Munaziri wa Mungu tangu kuzaliwa kwake. Naye ataanza kuwakomboa Waisraeli toka katika mikono ya Wafilistini.”


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.


Yeye hahitaji kutoa sadaka kila siku kama vile Makuhani wengine Wakubwa, kwanza kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kisha kwa ajili ya zambi za watu. Kwa maana amefanya vile mara moja tu wakati alipojitoa mwenyewe kufa.


Lakini, Mungu aliyenichagua mbele sijazaliwa na kuniita kwa neema yake, alipendezwa


Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”


kwa maana atahesabiwa kuwa mutu mukubwa mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kinywaji kikali, na atajazwa na Roho Mutakatifu tangu kuzaliwa kwake.


Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.


Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.


hakuweza kuvumilia, akamufunulia siri yake, akisema: “Nywele zangu hazijapata kunyolewa hata kidogo. Mimi nimewekwa Munaziri wa Mungu tangu katika tumbo la mama yangu. Kama nikinyolewa nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu akifanya kiapo cha kumutolea Yawe mwanadamu, mutu huyu anaweza kuondoa kiapo chake kwa kulipa kipimo cha feza kinachokadiriwa kama hivi:


Kwa sababu mimi Yawe ni mutakatifu, nami nimewatenga ninyi na mataifa mengine kusudi mukuwe mali yangu, mutakuwa watakatifu.


Maana namna gani itajulikana kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee kati ya watu wote katika dunia.


Paulo akaendelea kule Korinto kwa muda wa siku nyingi. Kisha akaagana na wandugu waamini, akasafiri kwa njia ya chombo na kwenda katika inchi ya Suria. Nao Prisila na Akila walikuwa pamoja naye. Mbele ya kuondoka, Paulo alinyolewa kwenye kivuko cha Kenkurea, kwa maana alikuwa ametimiza kiapo alichofanya mbele ya Mungu.


Yawe akamwambia Musa:


Kwa hiyo ukuwe mwangalifu, usikunywe divai au kileo wala usikule kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu,


Lakini wao wakajibu: Sisi hatukunywi divai, maana Yonadabu mwana wa Rekabu, babu yetu, alituamuru hivi: Musikunywe divai; musikunywe ninyi wenyewe wala wana wenu milele.


Mutu akiahidi mbele ya Yawe au akifanya kiapo, anapaswa kutimiza ahadi yake. Anapaswa kushika yale yote aliyotamka kwa kinywa chake.


asionje mazao yoyote ya muzabibu, wala asikunywe divai au kileo wala kula chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu. Yote niliyomwamuru, ayafuate.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite