Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 5:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Kisha kuhani ataandika laana hizi katika kitabu na kuzisafisha katika maji machungu.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 5:23
14 Referans Kwoze  

Nikaona wale waliokufa, wakubwa na wadogo wakisimama mbele ya kile kiti cha kifalme. Vitabu vikafunguliwa na kitabu kingine kikafunguliwa ndicho kitabu cha uzima. Wale waliokufa wakahukumiwa kufuatana na matendo yao sawa vile ilivyoandikwa katika vitabu.


Basi mugeuke toka katika zambi, mumurudilie Mungu, kusudi awasamehe zambi zenu.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Unitakase kwa hisopo, nikuwe safi, unisafishe, nikuwe mweupe pee.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea wakati nabii Natani alipomufikia kwa kumwonya juu ya uzinzi alioufanya na Batiseba.


Heri kungekuwa mutu wa kunisikiliza! Ninaweza kutia sahihi yangu katika kila neno nililosema. Mungu Mwenye Uwezo anijibu! Heri mashitaki waadui zangu wanayonitolea yangeandikwa!


Yawe anasema hivi: ‘Angalia nitaleta uovu juu ya Yerusalema na juu ya wakaaji wake, laana zote zilizoandikwa katika kitabu kilichosomwa mbele ya mufalme wa Yuda.


“Sasa, andika wimbo huu, uwafundishe watu wa Israeli kusudi ukuwe ushuhuda wangu juu yao.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Uandike jambo hili katika kitabu, likuwe ukumbusho. Tena umwambie Yoshua kwamba nitawafuta kabisa Waamaleki katika dunia.”


Maji haya yanayoleta laana yaingie ndani ya tumbo lako na kukufanya tasa na tumbo lako livimbe. Naye mwanamuke ataitikia: Amina! Amina!


Atamukunywesha mwanamuke hayo maji machungu yanayaleta laana nayo yataingia ndani yake na kumuletea maumivu makali.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite