Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 4:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Basi, kwa kuwaepusha wasipate kuuawa kwa kukaribia vyombo hivyo vitakatifu sana utafanya hivi: Haruni na wana wake wataingia na kumupangia kila mumoja wao mapaswa yake na kazi yake.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 4:19
6 Referans Kwoze  

Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.


Tena wakati wa hema kuongolewa, Walawi ndio watakaoliongoa. Na wakati wa hema kusimikwa, Walawi ndio watakaolisimamisha. Kama mutu ambaye si Mulawi analikaribia, atauawa.


Musiache ukoo wa jamaa za Kohati kati ya Walawi uangamizwe.


Walipofika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Nakoni, Uza aliunyoosha mukono wake na kuligusa Sanduku la Mungu kwa sababu wale ngombe walijikwaa.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Shuka chini uwaonye watu wote wasikuje kuniona. Kama sivyo wengi wao wataangamia.


Wao watafanya kazi utakazowapa na kutimiza mapaswa yao juu ya hema. Lakini hawana ruhusa ya kugusa vyombo vya hema, wala kukaribia mazabahu, kusudi wasikufe, nawe vilevile usikufe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite