Aliikomboa inchi yote iliyokuwa mali ya Israeli, kutokea Pito la Hamati mpaka bahari ya Chumvi. Hivi ndivyo Yawe alivyoahidi kwa njia ya mutumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gati-Heferi.
Lakini kundi la waaskari la Wakaldea liliwafuatilia na kumukamata Zedekia karibu na Yeriko. Kisha kumukamata walimufikisha kwa Nebukadneza, mufalme wa Babeli huko Ribla, katika inchi ya Hamati, naye akamuhukumu.
Enyi Waisraeli, kweli nitaleta taifa moja likuje kuwashambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nalo litawatesa ninyi kuanzia Hamati upande wa kaskazini, mpaka kwenye kijito cha Araba, upande wa kusini.
Kwa hiyo, Daudi akawakusanya Waisraeli wote katika inchi, tokea kwenye kijito cha Sihori kinachokuwa Misri, mpaka kwenye kiingilio cha Hamati kwa kulileta Sanduku la Agano toka Kiriati-Yearimu.