16 Yawe akamwambia Musa:
Makabila hayo mawili na nusu yamepata urizi wao ngambo ya muto Yordani upande wa mashariki, kuelekea Yeriko, jua linakotokea.
Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni ndio watakaowagawanyia watu inchi kuwa mali yao.
Haya ndiyo maeneo ya inchi ambayo Waisraeli walipewa katika inchi ya Kanana. Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na wakubwa wa ukoo za makabila ya Waisraeli waliyowagawanyia Waisraeli.
Kule Shilo, Yoshua akazipigia kura sehemu hizo mbele ya Yawe, akawagawanyia Waisraeli; kila kabila na sehemu yake.
Kwa hiyo hamutagawanyiwa sehemu yoyote ya inchi kati ya watu wa Yawe.