Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 34:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 halafu utateremuka kufuata muto Yordani mpaka bahari ya Chumvi hii ndiyo itakuwa inchi yako kama vile mupaka unavyokuwa.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 34:12
10 Referans Kwoze  

Upande wa kusini mupaka wenu utakuwa kutoka jangwa la Sini kupitia upande wa Edomu. Utaanzia mashariki upande wa kusini mwisho wa bahari ya Chumvi.


Wafalme wale watano waliyaunganisha majeshi yao katika bonde la Sidimu, ni kusema bahari ya Chumvi.


Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).


Kutoka Sefamu utaelekea kusini mpaka Ribla, upande wa mashariki wa Aini; kisha mupaka huo utakwenda chini mpaka kwenye muteremuko wa upande wa mashariki wa ziwa la Kinereti,


Basi, Musa akawaambia Waisraeli: Hii ndiyo inchi mutakayoirizi kwa kupiga kura, inchi ambayo Yawe ameagiza ipewe kwa makabila tisa na nusu.


Mipaka ya inchi yenu itakuwa kutoka bahari Nyekundu mpaka bahari ya Mediteranea na kutoka jangwa mpaka muto Furati. Nitawatia wakaaji wa inchi ile katika mikono yenu, nanyi mutawafukuza wawaondokee.


Wakati huu, Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi. Basi, Yawe akamwambia: “Wewe sasa umekuwa muzee wa miaka mingi, na kumebaki bado sehemu kubwa za inchi ambazo hazijatwaliwa.


Mupaka wao wa upande wa mashariki ni bahari ya Chumvi mpaka pale muto Yordani unapoingilia katika bahari. Na mupaka wao upande wa kaskazini ulipita kutokea pembe ya bahari ya Chumvi pahali ambapo muto Yordani unaingilia katika bahari.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Hii ndiyo mipaka ya inchi mutakayoigawanyia makabila kumi na mawili ya Waisraeli. Lakini kabila la Yosefu lipewe mara mbili.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite