Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 34:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kutoka Sefamu utaelekea kusini mpaka Ribla, upande wa mashariki wa Aini; kisha mupaka huo utakwenda chini mpaka kwenye muteremuko wa upande wa mashariki wa ziwa la Kinereti,

Gade chapit la Kopi




Hesabu 34:11
16 Referans Kwoze  

Kusudi asiendelee kutawala akiwa kule Yerusalema, Neko mufalme wa Misri alimufunga kule Ribla katika inchi ya Hamati, akawalipisha watu wa Yuda kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza na kilo makumi tatu na ine za zahabu.


Upande wa magaribi, inchi yao ilienea mpaka muto Yordani. Toka ziwa Galilaya upande wa kaskazini, ukashuka mpaka kwenye bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, mpaka kwenye miteremuko ya Pisiga, upande wa mashariki.


na kwa wafalme waliokuwa katika milima ya upande wa kaskazini, waliokuwa Araba ambayo ilikuwa upande wa kusini wa Kineroti, kwenye mabonde na waliokuwa Nafoti-Dori katika upande wa magaribi.


Siku moja, Yesu alisimama pembeni ya ziwa la Genezareti na watu wengi walimusongasonga kusudi wasikie neno la Mungu.


Miji yao iliyokuwa na kuta ni: Zidimu, Zeri, Hamati, Rakati, Kinereti, Adama, Rama, Hazori, Kedesi, Edirei, Eni-Hazori, Ironi, Migdali-Eli, Horemu, Beti-Anati na Beti-Semesi. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na tisa pamoja na vijiji vyake.


Nyuma ya maneno hayo, Yesu akavuka ziwa la Galilaya (linaloitwa vilevile Tiberia).


Walipokwisha kuvuka ziwa, wakafika pande za Genezareti.


Kulekule Ribla, mufalme wa Babeli aliwaua wana wa Zedekia mbele ya baba yao. Aliwaua vilevile wakubwa wote wa inchi ya Yuda.


Basi, Wababeli wakamuteka mufalme, wakamupeleka kwa mufalme wao kule Ribla, naye akamuhukumu.


Vilevile miji iliyokuwa katika bonde la Beti-Haramu, Beti-Nimura, Sukoti na Zafoni na inchi yote iliyokuwa ya mufalme Sihoni wa Hesiboni; eneo hilo lilikuwa upande wa mashariki wa Yordani na kupakana na upande wa kusini wa bahari ya Kineroti.


Mupaka wenu wa upande wa mashariki mutauweka kutoka Hazari-Enani mpaka Sefamu.


halafu utateremuka kufuata muto Yordani mpaka bahari ya Chumvi hii ndiyo itakuwa inchi yako kama vile mupaka unavyokuwa.


Basi Wakaldea walimukamata mufalme, wakamupeleka kwa mufalme wa Babeli kule Ribla, katika inchi ya Hamati, naye akamuhukumu.


Vilevile, alitawala inchi yote ya Araba, kutokea bahari ya Kineroti, upande wa mashariki, mpaka Beti-Yesimoti kwenye bahari ya Chumvi na kuendelea mpaka chini ya mulima Pisiga.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite