Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 33:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hivi ndivyo vituo ambavyo Waisraeli wakapiga kambi walipotoka Misri wakiwa katika makundi ya makabila yao chini ya uongozi wa Musa na Haruni.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 33:1
11 Referans Kwoze  

Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.


Wewe ukajifanyia njia juu ya bahari; ulitembea juu ya maji yale mengi, lakini pahali ulipopita hapakuonekana.


“Yakobo na jamaa yake walipokwenda Misri, na Wamisri walipowagandamiza, babu zenu walimulilia Yawe. Naye akawatuma Musa na Haruni ambao waliwatoa babu zenu katika inchi ya Misri na kuwafanya mukae katika inchi hii.


Nyuma nikawatuma Musa na Haruni, nikailetea inchi ya Misri mapigo, na kisha nikawatoa ninyi katika inchi ile.


Pahali pake, Mungu akawapitisha Waisraeli katika njia ya muzunguko kupitia katika jangwa, kuelekea bahari Nyekundu. Waisraeli wakaondoka katika inchi ya Misri wakiwa wamejitayarisha kwa vita.


Siku hiyohiyo Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri kwa makundi.


Waisraeli waliondoka katika muji wa Ramesesi, wakasafiri kwa miguu kuelekea Sukoti. Walikuwa wanaume yapata elfu mia sita, bila kuhesabu wanawake na watoto.


Musa aliandika jina la kila pahali walipopiga kambi, kituo kwa kituo, kwa agizo la Yawe.


Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.


Haruni na Musa ndio walioambiwa na Yawe: “Mutoe watu wa Israeli kutoka inchi ya Misri, vikundi kwa vikundi.”


Katika siku ya mwisho ya mwaka wa mia ine na makumi tatu, siku ileile ndipo makabila yote ya Yawe yaliondoka katika inchi ya Misri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite