Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Utamupatia Haruni Walawi na wazao wake makuhani; hao wametolewa kwake kabisa kati ya Waisraeli.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 3:9
15 Referans Kwoze  

na nimewatoa kwa Haruni na wana wake, kama vile zawadi kutoka kwa Waisraeli, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano kwa ajili ya Waisraeli na kuwafanyia upatanisho kusudi kusitokee pigo kati ya Waisraeli wakikaribia Pahali Patakatifu.


Ni yeye ndiye aliwapatia watu zawadi za kipekee. Amewaweka wamoja kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa watangazaji wa Habari Njema, wengine kuwa wachungaji na walimu.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Alipopanda juu, alikamata wafungwa, aliwapatia watu zawadi.”


Watatunza vyombo vyote vya hema la mukutano na kuwasaidia Waisraeli wanapofanya kazi zao kwenye hema takatifu.


Hao wametolewa wakuwe wangu kabisa, pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli.


Munaona ni jambo dogo kwenu kwamba Mungu wa Israeli amewachagua ninyi kati ya Waisraeli wote, kusudi muweze kumukaribia na kutumika katika hema la Yawe na kushugulika na kutumikia Waisraeli wote?


Hivi ndivyo utakavyowatenga Walawi kati ya Waisraeli wengine kusudi wakuwe wangu.


Sasa ninawatwaa Walawi pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli,


Wewe, wana wako na wazao wako wote mutatumika kama vile makuhani; wandugu zako wengine wa kabila lako watafanya kazi pamoja nawe mbele ya hema la kuchunga vibao vya agano.


Ndugu zao wengine walipewa kazi zingine katika hema takatifu la nyumba ya Mungu.


Kisha akasema: “Hakuna mutu mwingine yeyote atakayebeba Sanduku la Agano isipokuwa Walawi, maana Yawe aliwachagua wao kwa kulibeba na kumutumikia kwa milele.”


Hizi ni ukoo za watumishi wa hekalu waliorudi kutoka katika uhamisho: Siha, Hasufa, Tabaoti, Kerosi, Siaha, Padoni, Lebana, Hagaba, Akubu, Hagabu, Semaya, Hanani, Gideli, Gahari, Raya, Resini, Nekoda, Gazamu, Uza, Pasea, Besayi, Asina, Munimu, Nefisimu, Bakuki, Hakufa, Harihuri, Basiluti, Mehida, Harsa, Barkosi, Sisera, Tema, Nezia, Hatifa.


Vilevile, kwa ajili ya kazi ya Mungu katika Yerusalema, waliwapanga makuhani katika makundi yao ya Walawi katika zamu zao kufuatana na maagizo yaliyoandikiwa katika kitabu cha Musa.


Zaidi ya hao, kulikuwa watumishi wa hekalu mia mbili makumi mbili ambao babu zao walikuwa wamechaguliwa na mufalme Daudi na wakubwa wake kwa kuwasaidia Walawi. Majina ya watu wote hawa yameandikwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite