Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Uwalete karibu watu wa kabila la Lawi, uwaweke mbele ya kuhani Haruni wapate kumutumikia.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 3:6
18 Referans Kwoze  

Hivyo mutajua kwamba nimewapa amri hii kusudi agano langu na ukoo wa Lawi likuwe la kudumu.


Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.


Lakini Walawi hawakuhesabiwa kati ya watu wa Israeli kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.


Halafu, kambi ya kabila la Walawi likiwa katikati ya kambi zote nao wakibeba hilo hema la mukutano wataondoka; kila kundi likisafiri kwa kufuata nafasi yake kwa bendera.


Yawe akamwambia Musa:


Kwa hiyo, ilikuwa ni kazi yao kutunza hema la kusanyiko na Pahali Patakatifu, na kuwasaidia wandugu zao makuhani, wazao wa Haruni, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe.


Basi wana wangu, musikuwe wavivu. Yawe amewachagua ninyi kusudi mumutumikie, muwaongoze watu wake katika ibada, na kumufukizia ubani.”


Vilevile, kwa ajili ya kazi ya Mungu katika Yerusalema, waliwapanga makuhani katika makundi yao ya Walawi katika zamu zao kufuatana na maagizo yaliyoandikiwa katika kitabu cha Musa.


Kuelekea Walawi, hao nimewapa sehemu ya kumi ya kila kitu Waisraeli wanachonitolea kuwa urizi wao. Haya yatakuwa malipo yao kwa kazi wanayotoa katika kulitunza hema la mukutano.


Ndugu zao wengine walipewa kazi zingine katika hema takatifu la nyumba ya Mungu.


Kisha akasema: “Hakuna mutu mwingine yeyote atakayebeba Sanduku la Agano isipokuwa Walawi, maana Yawe aliwachagua wao kwa kulibeba na kumutumikia kwa milele.”


Kazi yao ilikuwa ni kuwasaidia makuhani wa ukoo wa Haruni katika kazi ya kujenga nyumba ya Yawe, kutunza viwanja na vyumba, kusafisha vyombo vitakatifu vyote na kufanya kazi zinazoelekea kujenga nyumba ya Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite