Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 25:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ndivyo Waisraeli walivyojiunga na mungu Bali wa Peori, nayo hasira ya Yawe ikawaka juu yao.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 25:3
13 Referans Kwoze  

Yawe anasema: Nilipowakuta Waisraeli walikuwa kama zabibu katika jangwa. Nilipowaona babu zenu, walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza. Lakini walipofika kule Bali-Peori, wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali, wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.


Zambi tulizotenda kule Peori hazitoshi? Hamwoni kwamba bado hatujajitakasa na kwamba mateso yake bado yanaisumbua watu wa Yawe?


Itawabidi kuiacha hiyo inchi yenu niliyowapa, nami nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua, kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.


Nani anayetambua uzito wa hasira yako? Nani anayeona matokeo ya kasirani yako?


Kwa hiyo Yawe akawaka hasira juu ya Waisraeli, akasema: “Kwa sababu watu hawa wamevunja agano nililofanya na babu zao, wakakataa kutii sauti yangu,


Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawaacha wanyanganyi wanyanganye mali zao. Akawatoa kwa waadui zao waliowazunguka hata wasiweze tena kuwashinda.


Musa akawaambia waamuzi wa Israeli: Kila mumoja wenu amwue mutu yeyote kati yenu ambaye amejiunga na mungu Bali wa Peori.


Mukumbuke kwamba wanawake ndio waliofuata shauri la Balamu, wakasababisha Waisraeli wamwasi Yawe kule Peori hata ugonjwa mukali ukawafikia watu wa Yawe.


Basi, Waisraeli walitenda uovu mbele ya Yawe na kuabudu Mabali.


Walimwacha Yawe, wakatumikia Mabali na Mastaroti.


Lakini sitawaazibu wabinti zenu wanapofanya uzinzi, wala bibi-arusi wenu wanapofanya uasherati, maana, wanaume wenyewe ndio wanaofuatana na wazinzi, na kutambikia pamoja nao katika ibada za uzinzi. Watu hawa wenye kukosa akili hakika wataangamia!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite