Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”
Wewe Yuda, mwana wangu, ni kama mwana-simba ambaye amepata mawindo yake akapanda juu, kama simba mukali anajinyoosha na kulala chini. Simba dike, nani anayesubutu kumwamusha?
Kuja sasa uwalaani watu hawa kwa ajili yangu maana wana nguvu kuliko mimi. Labda nitaweza kuwashinda na kuwafukuza wasiingie katika inchi yangu, kwa maana unajua kwamba wewe ukimubariki mutu anabarikiwa, ukimulaani mutu analaaniwa.
Balaki akawaka hasira juu ya Balamu, akapiga mikono kwa kasirani na kumwambia: Nilikuita uwalaani waadui zangu, lakini mara hizi zote tatu umewabariki!
Yawe aliniambia hivi: Simba mukali ananguruma kwa kukinga nyama aliyemukamata; hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza, hatishiki kwa kelele zao, wala hashituki kwa sauti zao. Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.
Kulikuwa vilevile sanamu kumi na mbili za simba wamesimama, mumoja kwa mwisho wa kila ngazi. Kiti kama hicho kilikuwa bado hakijatengenezwa katika ufalme wowote.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na kiti cha kuegemea miguu cha zahabu, vyote hivyo vilikuwa vimeshikamanishwa na kiti hicho cha kifalme; na kila upande kilikuwa na pahali pa kuegemeza mikono tena kilikuwa na sanamu mbili za simba karibu na pahali pale pa kuegemeza mikono.
Kule akawaelezea Zeresi, muke wake, na warafiki zake wote mambo yote yaliyomupata. Zeresi na hao warafiki zake wakamwambia: “Ikiwa huyu Mordekayi, ambaye umeanza kupoteza madaraka yako kwa ajili yake ni wa kabila la Wayuda, basi, hautamuweza; atakushinda kabisa.”