Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 24:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Anasema yeye aliyesikia maneno ya Mungu, mutu aliyeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu, mutu anayeinama uso mpaka chini na kuona wazi.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 24:4
20 Referans Kwoze  

Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Siku moja ya kumwabudu Bwana, nikashikwa na Roho wa Mungu, nikasikia sauti kubwa, inayolia kama baragumu,


Ulionekana kama upindi wa mvua wakati wa mvua. Ulionekana kufanana na utukufu wa Yawe. Nilipouona, nilianguka uso mpaka chini, nikasikia sauti ya mutu mwenye kusema.


Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto.


“Nilipokuwa nimekwisha kurudia Yerusalema, na nilipokuwa nikiomba katika hekalu, nikapata maono.


Petro akiwa akifikiri juu ya maana ya yale maono, Roho Mutakatifu akamwambia: “Kuna watu watatu hapa wanaokutafuta.


Naye akasikia njaa, na kuhitaji chakula. Walipokuwa wakimutengenezea chakula, akakuwa sawa amezimia.


Ee Yawe, ngao yetu ni chini ya ulinzi wako. Mufalme wetu ametoka kwako, ewe Mutakatifu wa Israeli.


Alivua nguo zake, akatabiri mbele ya Samweli. Alibaki uchi kwa siku moja, muchana na usiku. Kwa hiyo watu walianza kujiuliza: “Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”


Hapo, Yawe akafungua macho ya Balamu, naye akamwona malaika wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa toka kifuko chake. Balamu akajitupa uso mpaka chini.


Basi, Mungu akamufikia Balamu usiku ule, akamwambia: Kama watu hawa wamekuja kukuita, kwenda pamoja nao, lakini fanya tu kile nitakachokuambia.


Jua lilipokuwa likitua, Abramu akashikwa na usingizi muzito. Hofu na giza nene vikamufunika.


Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Hema zenu zinapendeza sana, enyi watu wa Yakobo; hakika, kambi zenu, enyi watu wa Israeli!


Basi, Balamu akasema mashairi haya: Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Beori, mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho,


Halafu, Mikaya akasema: “Niliona watu wote wa Israeli wametawanyika juu ya milima kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Naye Yawe akasema: ‘Watu hawa hawana kiongozi. Basi warudi kila mutu kwake kwa amani.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite