Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 23:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mungu akakutana naye. Balamu akamwambia: Nimetayarisha mazabahu saba na kutoa ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja juu ya kila mazabahu.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 23:4
12 Referans Kwoze  

Yawe akakutana na Balamu, akamupa maneno atakayosema, na kumwambia arudi kwa Balaki.


Si kwa matendo yenu, kusudi mutu asipate kujivuna.


Ninafunga kula chakula mara mbili kila juma na ninatoa fungu moja la kumi la vitu vyote ninavyopata.’


Basi sasa mutu ataweza kujivuna? Hapana! Kwa sababu gani? Kwa sababu anatii Sheria? Hapana. Lakini kwa sababu anamwamini Yesu.


Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.


Wakasema: ‘Watumishi hawa wa mwisho wametumika kazi kwa saa moja tu, nawe umewalipa sawasawa na sisi tuliovumilia muchoko na jua kali kwa muchana kutwa!’


Balamu akamwambia Balaki: Unijengee mazabahu saba hapa kisha uniletee ngombe dume saba na kondoo dume saba.


Basi, Mungu akamufikia Balamu usiku ule, akamwambia: Kama watu hawa wamekuja kukuita, kwenda pamoja nao, lakini fanya tu kile nitakachokuambia.


Kisha Mungu alimufikia Balamu, akamwuliza: Ni nani hawa wanaokaa nawe?


Halafu Balamu akamwambia Balaki: Baki hapa karibu na sadaka yako ya kuteketezwa kwa moto, nami niende. Labda Yawe atakutana nami. Chochote atakachonionyesha nitakuja kukuambia. Basi, Balamu akaenda peke yake juu ya kilele cha mulima.


Yawe akamupa Balamu maneno atakayosema na kumwambia arudi kwa Balaki.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite