Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 23:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kisha, Balaki akamwambia Balamu: Tuende pahali pengine ambapo utaweza kuwaona; hata hivyo utaona tu sehemu yao, hautaweza kuwaona wote. Kisha uwalaani kutoka huko kwa ajili yangu.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 23:13
10 Referans Kwoze  

Yeye alipenda kulaani watu; laana imupate yeye mwenyewe. Hakuwatakia wengine baraka; basi, asipate baraka yeye mwenyewe.


Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!


Halafu, mutu mumoja wa Mungu akamukaribia mufalme wa Israeli, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu Waaramu wamesema kwamba mimi Yawe ni Mungu wa milima wala si Mungu wa inchi ya bonde, nitakupa ushindi juu ya kundi hili kubwa, nawe utatambua kwamba mimi ni Yawe.’ ”


Watumishi wa mufalme Beni-Hadadi walimushauria hivi: “Miungu ya Waisraeli ni miungu ya juu ya milima; ndiyo maana tulishindwa. Lakini, bila shaka tutawashinda kama tukipigana nao katika bonde.


Naye Balaka mwana wa Sipori, mufalme wa Moabu, akakuja na kuwashambulia Waisraeli. Akamwalika Balama mwana wa Beori akuje kuwalaani ninyi.


Kesho yake, Balaki akamutwaa Balamu, akapanda naye mpaka Bamoti-Bali; kutoka huko, Balamu aliweza kuwaona wamoja kati ya Waisraeli.


Balamu akamwambia Balaki: Hainipasi tu kusema maneno Yawe aliyoweka ndani ya kinywa changu?


Basi, Balaki akamutwaa Balamu kwenye shamba la Sofimu, juu ya kilele cha mulima Pisiga. Hapo akajenga mazabahu saba na kutoa juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


Kuja sasa uwalaani watu hawa kwa ajili yangu maana wana nguvu kuliko mimi. Labda nitaweza kuwashinda na kuwafukuza wasiingie katika inchi yangu, kwa maana unajua kwamba wewe ukimubariki mutu anabarikiwa, ukimulaani mutu analaaniwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite