Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 22:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Hasira ya Mungu ikawaka kwa sababu Balamu alikuwa anakwenda; hivyo malaika wa Yawe akakutana naye katika njia. Wakati huo Balamu alikuwa amepanda juu ya punda wake naye alisindikizwa na watumishi wake wawili.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 22:22
11 Referans Kwoze  

Malaika wa Yawe akamwambia Balamu: Mbona umemupiga punda wako mara tatu? Nimekuja kukuzuia, kwa sababu njia yako ni mbaya.


Akiwa bado katika njia kurudi Misri, Musa alikuwa pahali pa kulala pa wageni. Basi, Mungu akakutana naye na kutaka kumwua.


Amevuta upinde wake kama adui, na kuuweka mukono wake wa kuume tayari, amewaua wote waliopendeza macho. Amemwanga hasira yake kama moto katika hema yetu watu wa Sayuni.


Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.


Yehu akaamuru: “Mutangaze mukutano wa ibada ya Bali!” Tangazo likatolewa,


Lakini malaika wa Yawe akamwambia Balamu: Kwenda na watu hawa, lakini utasema tu kile nitakachokuambia. Basi, Balamu akaendelea na safari pamoja na viongozi wa Balaki.


Muangalie, mimi ninamutuma malaika awatangulie katika safari kusudi awalinde na kuwafikisha katika inchi niliyowatayarishia.


Basi, punda akamwona malaika huyo wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa. Kwa hiyo akaacha njia, akaenda pembeni. Balamu akamupiga huyo punda, akamurudisha katika njia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite