Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 21:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Waisraeli wakafunga safari kutoka mulima Hori, wakapitia njia inayoelekea bahari Nyekundu kusudi wazunguke inchi ya Edomu. Lakini katika njia watu wakavunjika moyo.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 21:4
14 Referans Kwoze  

Musa akawaelezea Waisraeli maneno hayo. Lakini wao hawakumusikiliza kwa sababu walikuwa wamekufa moyo kutokana na utumwa mukali.


Kisha wakasafiri wakipitia katika jangwa kuzunguka inchi ya Edomu na Moabu mpaka walipofika upande wa mashariki wa Moabu, wakapiga kambi ngambo ya muto Arnoni. Lakini hawakuingia katika eneo la Moabu. Muto Arnoni ndio uliokuwa mupaka wa Moabu.


Mbona munawavunja moyo Waisraeli wasiende katika inchi ambayo Yawe amewapa?


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Kutoka mulima Hori, Waisraeli wakapiga kambi yao Salmona.


Wao walikwenda mpaka bonde la Eskoli, wakaiona inchi, lakini waliporudi, wakavunja Waisraeli moyo kusudi wasiingie katika inchi Yawe aliyowapa.


Lakini ninyi, mugeuke na kurudi katika jangwa kuelekea bahari Nyekundu.’


Musa akafanya kama vile alivyoamriwa na Yawe. Wote watatu wakapanda juu ya mulima mbele ya watu wote wengine.


Kwa sababu Waamaleki na Wakanana wanakaa katika mabonde ya inchi hiyo, kesho mugeuke nyuma muende katika jangwa kuelekea bahari ya Shamu.


“Kisha, tukageuka, tukasafiri katika jangwa kwa kupitia njia ya bahari Nyekundu, kama vile Yawe alivyoniambia. Tukatangatanga karibu na mulima Seiri kwa muda murefu.


Tutashambulia kutokea upande gani?” Yoramu akajibu: “Tutashambulia kutokea jangwa la Edomu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite