Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.
Dada yako mukubwa ni Samaria, aliyekaa upande wako wa kaskazini pamoja na wabinti zake. Dada yako mudogo ni Sodoma, aliyekaa upande wako wa kusini pamoja na wabinti zake.
Wakimbizi wanaochoka wanasimama chini ya kivuli cha Hesiboni. Moto umewaka huko katika muji; ulimi wa moto toka nyumba ya kifalme ya Sihoni; umeteketeza mipaka ya Moabu, umeunguza milima ya hao wanaopiga kelele.
Kilio cha watu wa Hesiboni kinasikilika huko Eleale mpaka Yasa; kinaenea kutoka Soari mpaka Horonaimu na kufika hata Eglati-Selisia. Hata maji ya kijito Nimurimu yamekauka.
utukufu wa inchi ya Moabu umetoweka. Mupango ulifanywa huko Hesiboni juu yake: Basi! Tuwaangamize wasikuwe tena taifa! Nawe muji wa Madimeni utanyamazishwa, upanga utakufuatilia.
Wahori vilevile waliishi huko Seiri zamani, lakini wazao wa Esau wakawafukuza na kuwaangamiza, kisha wao wenyewe wakakaa katika eneo hilo pahali pao. Waisraeli wakafanya vile vile katika inchi ile ambayo Yawe aliwapa ikuwe mali yao.)
Wakati wote Waisraeli walipoishi katika muji wa Hesiboni na vijiji vyake, na muji wa Aroeri na vijiji vyake pamoja na miji yote inayokuwa kwa ukingo wa muto Arnoni kwa muda wa miaka mia tatu, kwa nini haukulikomboa eneo hilo wakati huo?
Kisha niliwaongoza mpaka katika inchi ya Waamori ambao waliishi upande mwingine wa muto Yordani. Walipigana nanyi, lakini mimi niliwapa ushindi juu yao mukawaangamiza na kuiteka inchi yao.