Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 20:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Hapo, Musa na Haruni wakaondoka kwenye mukutano wa watu, wakaenda kusimama kwenye mulango wa hema la mukutano, wakainama uso mpaka chini. Basi, utukufu wa Yawe ukawatokea,

Gade chapit la Kopi




Hesabu 20:6
15 Referans Kwoze  

Hapo, Musa na Haruni wakaanguka uso mpaka chini mbele yao.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Naye Kora akawakusanya watu wote pamoja, wakasimama mbele ya Musa na Haruni ambao walikuwa kwenye mulango wa hema la mukutano. Halafu utukufu wa Yawe ukawatokea watu wote.


Musa aliposikia hayo, akajitupa uso mpaka chini.


Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”


Daudi akainua macho yake, akamwona yule malaika wa Yawe akisimama kati ya mbingu na dunia, naye akiinua upanga wake juu ya Yerusalema tayari kuangamiza. Halafu Daudi na wazee wote walikuwa wakivaa nguo ya gunia, wakaanguka uso mpaka chini.


Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.


Lakini wengine wote pamoja wakatishia kuwapiga mawe. Kwa rafla, utukufu wa Yawe ukatokea juu ya hema la mukutano, mbele ya watu wote wa Israeli.


Hapo Yawe akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye mulango wa hema, akawaita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakasogea mbele.


Basi, Musa akamulilia Yawe akisema: “Nitawafanyia nini watu hawa? Wako karibu kunipiga mawe!”


Wakati Haruni alipokuwa akizungumuza na Waisraeli wote pamoja, watu wote wakaangalia kule katika jangwa na mara moja utukufu wa Yawe ukaonekana katika mawingu.


naye Yawe akamwambia Musa:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite