Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 20:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kisha Musa akainua mukono wake, akapiga lile jiwe mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika kwa wingi, watu wakakunywa pamoja na mifugo yao.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 20:11
24 Referans Kwoze  

Wote walikunywa kinywaji kimoja cha kiroho; kwa maana walikunywa maji yaliyotoka ndani ya lile jiwe lililosafiri pamoja nao, nalo jiwe lilikuwa Kristo.


Angalia mimi nitasimama mbele yako juu ya jiwe la mulima wa Horebu, nawe utapiga lile jiwe na maji yatabubujika kutoka mule kusudi watu wote wapate kunywa.” Basi, Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli.


Ni yeye aliyewaongoza katika lile jangwa kubwa na la kutisha, lenye nyoka wenye sumu na nge katika inchi ile yenye kukauka isiyokuwa na maji, aliwatolea maji kutoka kwenye jiwe gumu.


Twaa ile fimbo yako, kisha wewe na ndugu yako Haruni mukusanye watu wote pamoja. Halafu, mbele ya macho yao, uambie jiwe linalokuwa mbele ya macho yao litoe maji yake. Utawatoshea maji ndani ya jiwe watu wote na mifugo yao waweze kunywa.


Kwa maana mutu mwenye kasirani hawezi kutimiza mambo ya haki mbele ya Mungu.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Ni mimi niliyewachunga mulipokuwa katika jangwa, katika inchi iliyokuwa yenye kukauka.


Alitiririsha vijito kutoka katika jiwe, nayo maji kama mito.


Kwa sababu hamukulibeba safari ya kwanza, Yawe, Mungu wetu, akatuazibu maana hatukulitunza kama vile alivyoagiza.”


Saulo akamwambia Samweli: “Nimetenda zambi. Nimeasi amri ya Yawe na amri yako, kwa sababu niliwaogopa watu, nikawatii wao.


Kisha akasema: “Hakuna mutu mwingine yeyote atakayebeba Sanduku la Agano isipokuwa Walawi, maana Yawe aliwachagua wao kwa kulibeba na kumutumikia kwa milele.”


Kwa nini basi, haukuitii sauti ya Yawe? Kwa nini mukakimbilia vitu kwa kuvinyanganya na hivyo kutenda jambo ovu mbele ya Yawe?”


Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mumoja chetezo chake, wakaweka moto na ubani, wakamutolea Yawe moto usioruhusiwa, ambao haukulingana na agizo la Yawe.


Wewe umefanya chemichemi na vijito; na kukausha mito mikubwa.


Alipasua mawe kule katika jangwa, akawakunywesha maji kutoka shimo refu.


Ni kweli, alipiga jiwe, maji yakatiririka kama muto; lakini, sasa anaweza kweli kutupatia mukate, na kuwapatia watu wake nyama?”


Alipasua jiwe maji yakabubujika; yakatiririka katika jangwa kama muto.


anayegeuza jiwe kubwa kuwa ziwa, nalo jiwe gumu kuwa chemichemi za maji!


Muangalie, mimi ninafanya kitu kipya. Kinafanyika sasa hivi, nanyi mutaweza kukiona. Nitafanya njia katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa.


Alipowaongoza katika jangwa hawakuona kiu, aliwatiririshia maji kutoka katika jiwe, alipasua jiwe maji yakabubujika.


Mungu akafungua pahali palipokuwa shimo kule Lehi, akatiririsha maji. Samusoni akakunywa maji hayo na nguvu zake zikamurudilia. Chemichemi hiyo ikaitwa “Kisima cha Yule Anayeita” nayo iko kule Lehi mpaka leo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite