Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 19:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Haya ni masharti ya sheria ambayo mimi Yawe ninatoa. Uwaambie Waisraeli wawaletee ngombe dike mwekundu mukamilifu asiyekuwa na kilema chochote, na ambaye hajapata kufungwa nira.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 19:2
21 Referans Kwoze  

Kisha, wazee wa muji ule unaokuwa karibu zaidi na ile maiti watatwaa mwana-ngombe ambaye hajatumiwa kufanya kazi yoyote wala kutiwa nira.


Lakini mulikombolewa kwa njia ya damu yenye bei kali ya Kristo, aliyekuwa kama kondoo asiyekuwa na kilema wala uchafu.


Basi, mutayarishe gari jipya na ngombe wawili wenye kunyonyesha ambao bado hawajafungwa nira. Muwafunge kwenye gari hilo lakini vitoto vyao visiende pamoja nao, lakini vibaki katika zizi.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Yeye hakutenda zambi, wala neno la udanganyifu halikutoka ndani ya kinywa chake.


Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Aliyahesabu makosa yangu yote akayakusanya pahali pamoja; aliyafunga katika shingo langu kama nira, nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake. Yawe aliniweka katika mikono ya watu ambao siwezi kuwapinga.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Kuhani Eleazari akawaambia wanaume waliorudi toka kwa vita: Hii ndiyo sheria ambayo Yawe amemupa Musa.


Halafu kuhani atatwaa muti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu na kuvitia katika moto huo.


Kuhani atatwaa yule ndege mwingine muzima, kipande kile cha mwerezi, sufu ya rangi nyekundu na lile tawi la hisopo na kuvitumbukiza vyote katika damu ya yule ndege aliyechinjwa.


Mwana-kondoo yule asikuwe na kilema chochote, akuwe dume wa mwaka mumoja. Anaweza kuwa mwana-kondoo au mwana-mbuzi.


Yawe akawaambia Musa na Haruni:


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite