Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 18:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Ni mimi niliyewachagua wandugu zenu Walawi kati ya Waisraeli kama vile toleo kwenu. Wao wametengwa kwa ajili yangu mimi Yawe, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 18:6
14 Referans Kwoze  

Utamupatia Haruni Walawi na wazao wake makuhani; hao wametolewa kwake kabisa kati ya Waisraeli.


Sasa, utenge Walawi wote kuwa wangu pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli. Vilevile, utenge ngombe wa Walawi wote pahali pa wazaliwa wa kwanza wa ngombe wa Waisraeli. Mimi ni Yawe.


Sasa nimechagua Walawi kati ya Waisraeli wote, pahali pa kila muzaliwa wa kwanza mwanaume anayefungua tumbo la mama yake katika kila jamaa ya Israeli. Walawi ni wangu,


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitaamua kati ya kondoo wanono na kondoo zaifu.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Mimi –ni mimi!– nimesema na kumwita; nimemuleta, naye atafanikiwa katika mupango wake.


Vilevile nimemuchagua Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, afanye kazi pamoja naye. Vilevile nimewapa uwezo mukubwa watu wengine kwa ajili ya kazi mbalimbali, kusudi watengeneze vifaa vyote nilivyoagiza vifanywe:


Mimi nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao watawafuatilia katikati ya bahari. Nami nitajipatia utukufu kutokana na kuangamizwa kwa mufalme wa Misri na jeshi lake, magari yake ya vita pamoja na wapanda-farasi wake.


“Ninasimamisha agano langu nanyi na wazao wenu


Nitaleta mafuriko ya maji kwa kuangamiza viumbe vyote vyenye uzima katika dunia. Kila kiumbe chenye uzima katika dunia kitakufa.


Uwalete karibu watu wa kabila la Lawi, uwaweke mbele ya kuhani Haruni wapate kumutumikia.


maana kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri nilijitakasia kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli; kila muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu hata wa nyama; wao watakuwa wangu. Mimi ni Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite