Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 16:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Munaona ni jambo dogo kwenu kwamba Mungu wa Israeli amewachagua ninyi kati ya Waisraeli wote, kusudi muweze kumukaribia na kutumika katika hema la Yawe na kushugulika na kutumikia Waisraeli wote?

Gade chapit la Kopi




Hesabu 16:9
20 Referans Kwoze  

Basi, Isaya akamujibu: Musikilize basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Haitoshi kuwachokesha watu hata sasa munataka kumuchokesha Mungu wangu vilevile?


Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.


Wakati ule wakachagua watu wa kuchunga vyumba vya gala ambamo matoleo kwa ajili ya hekalu yaliwekwa, malimbuko ya kwanza, zaka na kuyakusanya kutoka katika mashamba ya miji, kwa ajili ya makuhani na Walawi kama ilivyotakiwa na Sheria. Watu wote wakafurahia makuhani na Walawi waliotumika,


Basi, watumishi hao wa Saulo walimwambia Daudi maneno hayo kwa siri, naye akawaambia: “Munazani mufalme kuwa baba mukwe wangu ni jambo dogo? Mimi ni mutu masikini na wa hali ya chini.”


Ni jambo dogo kwamba umetutoa Misri, inchi inayotiririka maziwa na asali, kusudi ukuje kutuua humu katika jangwa? Tena, unajifanya mukubwa wetu!


Uwalete karibu watu wa kabila la Lawi, uwaweke mbele ya kuhani Haruni wapate kumutumikia.


Lakini Walawi watapiga kambi zao kuzunguka hema la kuchunga vibao vya agano kusudi walilinde na kasirani yangu isiwake juu ya Waisraeli.


Wamoja kati yenu wanakula malisho mazuri na vilevile kukanyagakanyaga yale yaliyobaki. Wanakunywa maji safi na yanayobaki wanayachafua kwa miguu yao!


Pamoja na hayo, akawapa Walawi waliowafundisha watu wa Israeli na ambao walitakaswa kwa ajili ya Yawe, maagizo haya: “Muweke Sanduku takatifu ndani ya nyumba ambayo Solomono mwana wa Daudi, mufalme wa Israeli aliyojenga; hamuhitaji kulibebabeba tena juu ya mabega. Sasa mumutumikie Yawe, Mungu wenu, na watu wake Waisraeli.


Tena jambo hili lilikuwa dogo mbele ya macho yako. Zaidi ya hayo, Bwana wangu Yawe, umeahidi kuchunga jamaa yangu kwa miaka mingi inayokuja na kunijulisha hivyo, ee Bwana wangu Yawe.


Lakini Lea akamwambia kwa ukali: “Unazani ni jambo dogo kuninyanganya mume wangu na sasa unataka kutwaa dudai za mwana wangu?” Rakeli akamujibu: “Ikiwa utanipa dudai za mwana wako, Yakobo atalala kwako leo.”


Kwa ngambo yangu, si neno hata kidogo kuhukumiwa nanyi au na tribinali ya watu. Na hata mimi mwenyewe sijihukumu.


Siku moja walipokuwa wakifanya ibada, wakiwa wamefunga kula chakula, Roho Mutakatifu akasema: “Muwasimike Barnaba na Saulo kwa kazi ile niliyowachagulia.”


Utamupatia Haruni Walawi na wazao wake makuhani; hao wametolewa kwake kabisa kati ya Waisraeli.


Musa akaendelea kumwambia Kora: Musikilize, enyi Walawi!


Hao tu ndio watakaoingia katika hekalu langu, nao watakaribia kwenye mazabahu kwa kunitumikia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite