na wana wake Nemueli, Datani na Abiramu. Hawa wawili: Datani na Abiramu, ndio waliokuwa wamechaguliwa, lakini wakamupinga Musa na Haruni, na kujiunga na wafuasi wa Kora wakati walipomwasi Yawe.
Hao walimuvua nguo zake na kumwacha uchi. Waliwakamata watoto wake, naye mwenyewe wakamwua kwa upanga. Azabu hiyo aliyopata ikakuwa fundisho kwa wanawake wengine.
Hawa ndio waliokuwa wakubwa wa ukoo za kabila lile: Eferi, Isi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yadieli. Wote walikuwa waaskari shujaa, watu wenye heshima sana na viongozi katika ukoo hizo.
Katika siku zile na hata kisha, kulikuwa majitu katika dunia ambao walikuwa wazao wa wana wa Mungu na wabinti za wanadamu. Hao ndio watu waliokuwa mashujaa na wenye sifa wa zamani, na waliitwa Wanefili.
Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kutokana na uzuri wako, maana uzuri wako ulikamilika kwa sababu ya utukufu niliokujalia. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Baba yetu alikufia katika jangwa na bila mutoto yeyote mwanaume. Yeye hakukuwa kati ya wafuasi wa Kora waliokusanyika mbele ya Yawe, lakini alikufa kutokana na zambi yake mwenyewe. Hakukuwa na mutoto mwanaume.