Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 15:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mutanitolea mimi Yawe sadaka hii katika vizazi vyenu vyote vinavyokuja.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 15:21
8 Referans Kwoze  

Hivyo siku zote Waisraeli watatwaa sehemu hizo kutoka katika sadaka zao za amani wanazonitolea mimi Yawe na kumupa Haruni na wana wake. Hiyo ni sadaka yao kwa Yawe.


Tena utawaambia Walawi maagizo haya: Wakati mutakapopokea sehemu ya kumi ambayo Yawe amewapa kutoka kwa Waisraeli ikuwe urizi wenu, mutanitolea mimi Yawe sehemu moja ya kumi ya vitu hivyo.


Mbele ya siku hiyo ya kuniletea mimi Mungu wenu sadaka hiyo, hamuruhusiwi kula mazao ya kwanza ya mavuno yenu, yakuwe mabichi, yamekaangwa au yemepikwa kuwa mikate. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu pahali popote mutakapoishi.


Mutakapopika mukate, mukate wa kwanza wa mazao ya kwanza ya ngano yenu utatolewa kama sadaka kutoka pahali pa kupepetea ngano.


Lakini kama mutakosa kufuata amri zote ambazo mimi Yawe nimewapa kwa njia ya Musa,


Sehemu ya kwanza ya malimbuko yenu na vya matoleo yenu ya kila aina vitakuwa kwa ajili ya makuhani. Tena mutawapa sehemu ya kwanza ya unga wenu, kusudi mulete baraka juu ya nyumba zenu.


Mazao ya kwanza ya shamba lako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako. Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.


Kila unga wetu wa kwanza, matoleo yetu, matunda ya miti, divai na mafuta tutavileta kwa kuhani kwenye vyumba vya nyumba ya Mungu wetu. Tena tutaleta zaka zetu za mazao yetu kwa Walawi, maana ndio wanaoshugulika na kukusanya zaka zile katika vijiji vyetu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite