Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’
Yawe atawarudisha Misri kwa mashua, safari ambayo aliahidi kwamba hamungeifanya tena. Huko mutajaribu kujiuzisha kwa waadui zenu kuwa watumwa, lakini hakuna mutu atakayewanunua.”
lakini kwa muda wa mwezi muzima! Mutaikula mpaka iwatoke ndani ya pua, mpaka muichukie. Yote hayo ni kwa sababu mumemukataa Yawe anayekuwa hapahapa kati yenu, na kulia mbele yake mukisema: Kwa nini tulitoka Misri?