Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 14:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?

Gade chapit la Kopi




Hesabu 14:11
29 Referans Kwoze  

Kisha wakazarau inchi ile ya kupendeza, kwa sababu hawakuaminia ahadi ya Mungu.


Hata hivyo waliendelea kumukosea Mungu; ijapokuwa alitenda maajabu, hawakuamini.


kwa sababu hawakumwaminia, wala hawakutumainia kwamba angeweza kuwaokoa.


Lakini ingawa nilisema hayo yote, ninyi hamukumwamini Yawe, Mungu wenu,


musifanye mioyo yenu kuwa migumu kama babu zenu walivyofanya wakati walipomwasi Mungu, sawa siku ile walipomupima katika jangwa.


Ingawa vitambulisho vyote alivyoonyesha mbele yao, hawakumwamini,


Kundi hili la watu waovu litaendelea kuninungunikia mpaka wakati gani? Nimechoka na haya manunguniko ya Waisraeli juu yangu!


atakayeona inchi ile niliyoapa kuwapatia babu zao. Vilevile hata wale wanaonizarau hawataiona.


Tena ni watu gani Mungu aliowaapia kwamba hawataingia kwenye mapumziko aliyowatayarishia? Si wale waliokataa kumutii?


Ni watu gani waliosikia maneno ya Mungu na kumwasi? Si wale wote walioongozwa na Musa toka katika inchi ya Misri?


Hapo Yawe akamwambia Musa: “Mpaka wakati gani mutakataa kutii amri na sheria zangu?


Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.


Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kama nilivyokusudia kuwatendea ninyi maovu kwa sababu babu zenu walinikasirikisha wala sikuwaonea huruma,


Enyi watu wa Samaria, ninaichukia sanamu yenu ya mwana-ngombe. Hasira yangu inawaka juu yenu. Mutaendelea kuwa na makosa mpaka wakati gani?


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


“Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga? Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao, na wapumbafu kuchukia maarifa?


“Musikuwe wagumu kama kule Meriba, kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa,


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Ninawafahamu watu hawa. Wao wana vichwa vigumu.


Yawe akawaka hasira siku hiyo, akaapa akisema:


Watu hawa waovu wanakataa kusikia maneno yangu. Wanaendelea na kufuata mawazo yao wenyewe. Wanaifuata miungu mingine, wanaitumikia na kuiabudu. Hao watakuwa kama mukaba huu ambao haufai kitu.


Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.


Musikilize na kutii maneno atakayosema, wala musimwasi. Hatawasamehe uasi wenu maana nimemutuma kwa jina langu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite