Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 13:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 13:26
14 Referans Kwoze  

Hivi ndivyo walivyofanya babu zenu nilipowatuma kutoka Kadesi-Barnea kwa kupeleleza inchi.


Waisraeli wote wakafika katika jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza, wakapiga kambi yao huko Kadesi. Wakiwa huko, Miriamu akakufa na kuzikwa.


“Basi, kama vile Yawe, Mungu wetu, alivyotuamuru, tukaanza safari yetu kutoka mulima Horebu, tukapita katika lile jangwa kubwa la kutisha munalojua, kwa kufuata njia inayoelekea inchi ya milima ya Waamori. Tulipofika Kadesi-Barnea,


Waliondoka Esioni-Geberi, wakasafiri na kupiga kambi yao katika jangwa la Sini, ni kusema Kadesi.


Tukamulilia Yawe, naye akasikia kilio chetu, akatuletea malaika aliyetuondoa Misri. Sasa tuko hapa Kadesi, muji unaopakana na inchi yako.


Siku moja watu wa kabila la Yuda wakamwendea Yoshua kule Gilgali. Kalebu mwana wa Yefune, ambaye alikuwa Mukenizi, akamwambia Yoshua: “Bila shaka unakumbuka jinsi Yawe alivyomwambia Musa, mutu wa Mungu, juu yangu na wewe tulipokuwa Kadesi-Barnea.


Kisha wakarudi nyuma mpaka Enimisipati ni kusema Kadesi, wakapiga inchi yote ya Waamaleki, na kuwashinda Waamori waliokaa Hasasoni-Tamari.


Kisha kupeleleza inchi kwa muda wa siku makumi ine, watu hao wakarudi.


Musa akatuma wajumbe kutoka Kadesi kwa mufalme wa Edomu akamwambia: Ndugu yako Israeli anasema hivi: Wewe unajua taabu zote tulizozipata.


(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka mulima Horebu mpaka Kadesi-Barnea kwa njia ya mulima Seiri.)


Sauti ya Yawe inatetemesha jangwa, Yawe anatetemesha jangwa la Kadesi.


Basi, kwa agizo la Yawe, Musa akatuma watu kutoka jangwa la Parani. Watu wote waliotumwa walikuwa viongozi wa makabila mbalimbali ya watu wa Israeli.


Wao walikwenda mpaka bonde la Eskoli, wakaiona inchi, lakini waliporudi, wakavunja Waisraeli moyo kusudi wasiingie katika inchi Yawe aliyowapa.


Nilipokuwa na umri wa miaka makumi ine, Musa mutumishi wa Mungu, akanituma kutoka Kadesi-Barnea, kwenda kuipeleleza inchi. Niliporudi nikamuletea habari za mambo ya kule kadiri nilivyoamini katika moyo wangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite