Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 12:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Musa akamulilia Yawe akisema: Ninakusihi, ee Mungu, umuponye.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 12:13
23 Referans Kwoze  

Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


Usijiachilie kushindwa na ubaya, lakini ushinde ubaya kwa kutenda mema.


Muwaombee baraka wale wanaowalaani. Muwaombee wale wanaowaonea.


Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Uniponyeshe, ee Yawe, nami nitapona; uniokoe, nami nitaokoka; maana, wewe ndiwe sifa yangu.


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


Wakamunungunikia Musa na Haruni wakisema: Afazali tungekufia Misri! Afazali tungekufia hapahapa katika jangwa!


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


Kisha Abrahamu akamwomba Mungu, naye akamuponyesha Abimeleki, muke wake na wajakazi wake, hata wakaweza kupata tena watoto.


Kisha Mungu akamwambia: “Ingiza tena mukono wako kwenye kifua chako!” Musa akaingiza mukono wake kwenye kifua. Alipoutoa inje, ukarudilia hali yake ya kawaida kama vile mwili wake unavyokuwa.


Watu wakamulilia Musa, naye akamwomba Yawe na moto huo ukazimika.


Usimufanye Miriamu akuwe kama mutu aliyezaliwa mufu, ambaye karibu nusu ya mwili wake imeozeshwa.


Ninakutukuza, ee Yawe, maana umeniokoa, wala haukuwaacha waadui zangu wanisimange.


Yawe atamusaidia anapokuwa mugonjwa, atamuponyesha magonjwa yake yote.


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Basi, mufalme Yeroboamu akamwambia nabii: “Tafazali, umusihi Yawe, Mungu wako, uniombee mukono wangu upate kupona.” Naye nabii akamwomba Yawe, na mukono wa mufalme ukapona, ukarudia kwa hali yake ya zamani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite