Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 11:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Halafu Musa akamwambia Yawe: Kwa nini unanitendea vibaya mimi mutumishi wako? Mbona sikupata kukubaliwa mbele yako? Kwa nini umenibebesha muzigo wa kuwatunza watu hawa wote?

Gade chapit la Kopi




Hesabu 11:11
16 Referans Kwoze  

Lakini mimi peke yangu nitaweza namna gani kubeba muzigo wa kuamua matatizo yenu, mashitaki yenu na magomvi yenu?


Kisha Musa akamugeukia tena Yawe, akasema: “Ee Yawe, kwa nini unawatendea watu hawa uovu? Kwa nini hata ulinituma?


Na bila kutaja mambo yote mengine kama hayo, kila siku ninashugulika na makanisa yote.


Ninyi mumesema: Kumutumikia Mungu hakuna faida. Kuna faida gani kuyatii maagizo ya Yawe wa majeshi, au kujaribu kumwonyesha kwamba tumekosa mbele yake kwa kutembea kama watu wanaoomboleza?


Kwa nini mateso yangu hayaishi? Mbona kidonda changu hakiponi nacho hakitaki kutunzwa? Kama vile kijito chenye kukaukakauka, kisivyoweza kutumainiwa, ndivyo wewe umekuwa kwangu!


Ole wangu, mama yangu, kwa sababu ulinizaa! Mimi nimekuwa mutu wa ubishi na ugomvi katika inchi yote! Sijapata kukopesha mutu wala kukopeshwa na mutu, lakini kila mutu ananilaani.


Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako, maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.


Ee Yawe, kama ungekumbuka maovu yetu, nani, ee Bwana wetu, angeweza kuishi?


Nitamwambia Mungu: Usinitendee sawa na mwenye makosa. Unijulishe sababu ya kugombana nami.


Ikiwa hivi ndivyo utakavyonitendea, afazali uniue mara moja! Kama ninapata kukubaliwa mbele yako, usiniache kuendelea katika taabu yangu.


Basi, Musa akamulilia Yawe akisema: “Nitawafanyia nini watu hawa? Wako karibu kunipiga mawe!”


Musa akasikia watu wakilia katika jamaa zote, kila mutu kwenye mulango wa hema lake. Basi, hasira ya Yawe ikawaka sana; naye Musa akachukizwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite