Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 10:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Wakati wa vita katika inchi yenu juu ya waadui wanaowashambulia, mutatoa kitambulisho cha vita kwa kupiga baragumu hizi kusudi Yawe, Mungu wenu apate kuwakumbuka na kuwaokoa na waadui zenu.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 10:9
34 Referans Kwoze  

Walipofika aliwaambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Niliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri, nikawaokoa ninyi kutoka kwa Wamisri na falme zingine zilizowagandamiza.


Kila mara Yawe alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi yule, akawaokoa toka katika mikono ya waadui zao muda wote wa maisha ya mwamuzi yule. Ingawa hivyo, Yawe aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na masumbuko yao.


Kisha Mungu akamukumbuka Noa na nyama wote wa pori na wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo. Basi, Mungu akavumisha upepo juu ya inchi, maji yakaanza kupunguka.


Waadui zao waliwagandamiza, wakawatumikisha kwa nguvu.


Unikumbuke, ee Yawe, unapowaonyesha watu wako upendo. Unisaidie wakati unapowaokoa,


Watu wa Yuda walipoangalia nyuma, walishituka kuona wamezungukwa; basi wakamulilia Yawe, nao makuhani wakapiga baragumu zao.


Wasidoni, Waamaleki na Wamidiani waliwagandamiza nanyi mukanililia, nami nikawakomboa toka katika mikono yao.


Kwa miaka kumi na minane hao waliwatesa na kuwagandamiza Waisraeli walioishi kule Gileadi katika eneo la Waamori upande wa mashariki wa muto Yordani.


Watakapopiga hayo mabaragumu kwa mulio mukubwa na mara tu mutakaposikia huo mulio, watu wote watapiga kelele kubwa, nazo kuta za muji zitaanguka chini. Halafu watu wataushambulia muji kila mumoja kutoka pahali aliposimama.”


Musa akawapeleka kwa vita chini ya uongozi wa Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akiwa na vyombo vya Pahali Patakatifu na baragumu za kutoa kitambulisho.


Ngunga isipopigwa kwa mulio wa kuarifu, askari gani atakayeweza kujitayarisha kwa vita?


Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?


Kisha nikawawekea walinzi kwa kuwaarifu nikawaambia: Musikilize mulio wa baragamu. Lakini wao wakasema: Hatutausikiliza.


Mpaka wakati gani nitaendelea kuona bendera za vita na kusikia mulio wa baragumu?


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Mutoe tangazo, mupashe habari huko Yerusalema! Mupige baragumu kila pahali katika inchi! Mulalamike, mukisema: Mukusanyike pamoja! Mukimbilie katika miji yenye kuzungukwa na kuta!


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Enyi wakaaji wote katika ulimwengu, nanyi munaojaza dunia! Bendera itakaposimikwa kwenye mulima, muangalie! Baragumu itakapopigwa, musikilize.


Alitukumbuka wakati wa uzaifu wetu. Wema wake unadumu milele.


Lakini roho wa Yawe akamujaza Gideoni. Gideoni akapiga baragumu kwa kuwaita Waabiezeri wakuje kumufuata.


nikawakomboa toka katika mikono ya Wamisri wote waliowagandamiza. Nikawafukuza watu mbele yenu na kuwapa ninyi inchi yao.


Alipofika kule akapiga baragumu katika inchi ya milima ya Efuraimu, nao Waisraeli wakateremuka pamoja naye kutoka kule kwenye milima naye akawatangulia.


Siku hiyo ni ya mulio wa baragumu ya vita, juu ya miji yenye vikingio na kuta ndefu.


Mupige baragumu kule Gibea, na ngunga kule Rama. Mupige kelele la kujulisha hatari kule Beti-Aweni. Enyi watu wa Benjamina, adui yenu yuko nyuma!


Baragumu imepigwa na kuwafanya wote wakuwe tayari. Lakini hakuna anayekwenda kwa vita, kwa maana kasirani yangu iko juu ya watu wote.


Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.


Uwaambie watu wa Israeli hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa saba mutafanya siku ya mapumziko, siku ya ukumbusho itakayotangazwa kwa mulio wa baragumu na kufanya mukutano mutakatifu.


Na muangalie, Mungu mwenyewe ndiye kiongozi wetu na makuhani wake wako na baragumu zao tayari kuzipiga kwa kupana kitambulisho cha kuanza vita juu yenu. Enyi watu wa Israeli, muache kupigana vita na Yawe, Mungu wa babu zenu. Hamuwezi kushinda!”


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitavumisha sauti ya vita juu ya Raba muji wa Waamoni. –Ni ujumbe wa Yawe.– Raba utakuwa lundo la uharibifu, vijiji vyake vitateketezwa kwa moto. Halafu Israeli atatwaa tena urizi wake. Ni Yawe anayesema hivyo.


“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite