Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 1:51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

51 Tena wakati wa hema kuongolewa, Walawi ndio watakaoliongoa. Na wakati wa hema kusimikwa, Walawi ndio watakaolisimamisha. Kama mutu ambaye si Mulawi analikaribia, atauawa.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 1:51
15 Referans Kwoze  

Musa na Haruni na wana wao watapiga kambi yao mbele ya hema takatifu upande wa mashariki, ni kusema mbele ya hema la mukutano kuelekea upande linakotokea jua. Kazi yao itakuwa kutumika kwenye Pahali Patakatifu kwa jambo lolote lililohitajika kufanyika kwa ajili ya Waisraeli. Mutu mwingine yeyote aliyesogea karibu alipaswa kuuawa.


Utachagua Haruni na wana wake kusudi waweze kutimiza kazi zao za ukuhani; lakini kama mutu yeyote mwingine akikaribia, atauawa.


Halafu, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Uza. Mungu akamwua palepale. Uza akakufa palepale pembeni ya Sanduku la Mungu.


Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.


Na tangu sasa, watu wengine wa Israeli wasikaribie hema la mukutano kusudi wasitende zambi na kujiletea kifo.


Katika siku ya makumi mbili ya mwezi wa pili, mwaka wa pili tangu watu wa Israeli walipoondoka Misri, wingu lililokuwa juu ya hema la kuchunga vibao vya agano likainuliwa,


Alipofanya hivyo, pigo hilo likakoma, naye akabaki katikati ya waliokufa na waliokuwa wazima.


Wao watafanya kazi utakazowapa na kutimiza mapaswa yao juu ya hema. Lakini hawana ruhusa ya kugusa vyombo vya hema, wala kukaribia mazabahu, kusudi wasikufe, nawe vilevile usikufe.


Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.


Hili lilikuwa onyo kwa Waisraeli kwamba mutu yeyote ambaye si kuhani, maana yake asiyekuwa wa ukoo wa Haruni asiende kwenye mazabahu kwa kumufukizia Yawe ubani. Kama sivyo ataangamizwa kama Kora na wafuasi wake. Haya yote yalitendeka kama vile Yawe alivyomwambia Eleazari kwa njia ya Musa.


Wao watajiunga nawe katika kazi na kutimiza mapaswa yao kwa ukamilifu juu ya kazi zote za hema, wala kusikuwe mutu mwingine atakayekukaribia mule.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite