Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kiongozi mumoja wa jamaa kutoka kila kabila atakusaidia kufanya hesabu.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 1:4
19 Referans Kwoze  

Hao viongozi waliochaguliwa kati ya watu wa Israeli walikuwa vilevile viongozi wa jeshi.


Basi, akachagua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu makumi tano na watu kumikumi.


Finehasi akaondoka pamoja na wakubwa kumi, kila mumoja akiwa mukubwa wa jamaa katika kabila lake.


Hivyo nikatwaa wale viongozi wenye hekima, akili na ujuzi ambao muliwachagua kutoka katika makabila yenu, nikawaweka kuwa viongozi wenu. Nikawaweka wengine kuwa majemadari wa makundi ya watu elfu moja moja, ya watu mia moja moja, ya watu makumi tano tano na ya watu kumi kumi. Nikachagua vilevile wakubwa wengine wa kuchunga kila kabila.


Huyo Mwisraeli aliyeuawa pamoja na mwanamuke wa Kimidiani aliitwa Zimuri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa moja katika kabila la Simeoni.


Basi, Yawe akamwambia Musa: Utwae viongozi wote wa Israeli, uwatundike mbele yangu jua kati, kusudi kasirani yangu juu yenu ipite.


Vimekuwa vitakatifu kwa sababu watu hawa walivileta kwenye mazabahu ya Yawe. Basi, utwae vyetezo vya watu hao waliouawa kwa sababu ya zambi zao, vifuliwe kuwa vyembamba kusudi vikuwe kifuniko cha mazabahu. Hili litakuwa onyo kwa Waisraeli wote.


Lakini juu ya mambo mengine, chagua kati ya watu wote, watu wanaostahili, watu wanaomwogopa Mungu, waaminifu na wanaochukia kituliro. Uwape hao mamlaka, wakuwe na kazi ya kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, makumi tano na kumikumi.


Basi, Musa akawaambia Waisraeli kila kitu kama vile Yawe alivyomwamuru.


Basi, mufalme Solomono akawakusanya mbele yake kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila na wa ukoo za Waisraeli kusudi waliondoe Sanduku la Agano la Yawe katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni.


Hao ndio watu waliokuwa wamehesabiwa ambao Musa na Haruni waliwahesabu wakisaidiwa na wale viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila kiongozi akisimamia ukoo wake.


Basi, Musa, Haruni na viongozi wa Waisraeli wakafanya hesabu ya watu wa ukoo wa Kohati, kufuatana na jamaa zao,


Viongozi wa Israeli na wakubwa wa ukoo na viongozi wa makabila ambao walisimamia watu wale waliohesabiwa,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite