Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, mwaka wa pili nyuma ya watu wa Israeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa ndani ya hema la mukutano katika jangwa la Sinai, akamwambia hivi:

Gade chapit la Kopi




Hesabu 1:1
15 Referans Kwoze  

Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.


Siku ya kwanza ya mwezi wa tatu tangu walipotoka katika inchi ya Misri, watu wa Israeli wakafika katika jangwa la Sinai.


Kisha katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili nyuma ya Waisraeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa katika jangwa la Sinai. Akamwambia:


Hizo ndizo amri ambazo Yawe alimwamuru Musa kusudi awaambie Waisraeli kwenye mulima Sinai.


Yawe akamwita Musa na kuongea naye katika hema la mukutano, akamwambia:


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza mwaka wa pili kisha kutoka Misri, hema takatifu likasimikwa.


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, utasimika hema takatifu la mukutano.


Solomono alianza kujenga nyumba ya Yawe katika mwaka wa mia ine na makumi nane kisha Waisraeli kutoka Misri. Huo ulikuwa mwaka wa ine wa utawala wa Solomono juu ya Israeli, katika mwezi wa Zivu, ni kusema mwezi wa pili.


Na katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, wakakusanya Waisraeli wote. Waliandika majina ya wote wenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi, kulingana na jamaa zao na ukoo zao,


Walipoondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, kule wakapiga kambi mbele ya mulima Sinai.


Halafu kwa rafla, Yawe akawaambia Musa, Haruni na Miriamu: Mukuje katika hema la mukutano, ninyi watatu. Basi, wote watatu wakaenda kwenye hema la mukutano.


Siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, mwaka wa makumi ine nyuma ya kutoka Misri, Musa akawaambia watu kila kitu ambacho Yawe alimwamuru awaambie.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


Miaka makumi tatu na nane ilikuwa imepita tangu kuondoka Kadesi-Barnea mpaka kuvuka kijito Zeredi. Wakati huo, wote wenye umri wa kwenda kwa vita waliotoka Misri walikuwa wamekwisha kufa, kulingana na jinsi Yawe alivyowaapia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite