Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hagai 2:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Sema na Zerubabeli mutawala wa Yuda umwambie hivi: Nitazitikisa mbingu na dunia

Gade chapit la Kopi




Hagai 2:21
14 Referans Kwoze  

Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Nao Zerubabeli mwana wa Saltieli, na Yesua mwana wa Yosadaki, walipousikia ujumbe huo wakaanza tena kuijenga nyumba ya Mungu katika Yerusalema, wakisaidiwa na manabii wa Mungu.


Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupatia musaada kila asubui.


Basi, Yawe akamutia moyo mutawala Zerubabeli wa Yuda pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua na watu wote waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho. Wakaanza kazi hiyo ya kuijenga upya nyumba ya Yawe wa majeshi, Mungu wao,


Bwana wetu Yawe anasema hivi kwa Tiro: Wakaaji wa sehemu za kandokando ya bahari watatetemeka watakaposikia kishindo cha kuanguka kwako na mulio wa maumivu na wa watu wanaouawa.


Viongozi wao walikuwa Zerubabeli, Yesua, Nehemia, Seraya, Relaya, Mordekayi, Bilsani, Misipari, Bigwayi, Rehumu na Bana. Hii ndiyo hesabu ya watu wote wa ukoo za Waisraeli waliorudi kutoka katika uhamisho:


Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Simei. Wana wa Zerubabeli walikuwa: Mesulamu na Hanania. Alikuwa na binti mumoja, jina lake Selomiti.


Mushale ulioangukia kwa upande wa mukono wake wa kuume, ulionyesha Yerusalema. Pale wataweka vifaa vya vita kwa kuubomoa. Anaamuru mauaji, kelele za vita zipigwe, vifaa vya vita kwa kubomoa milango viwekwe, lundo ya udongo na minara kwa kuushambulia muji viwekwe vilevile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite