Watu walitoa feza za kuwalipa waseremala na wajengaji, walitoa vilevile chakula, vinywaji na mafuta, kusudi vipelekwe katika miji ya Tiro na Sidona kubadilishwa na miti ya mierezi kutoka Lebanoni. Miti hiyo ililetwa kwa njia ya bahari mpaka Yopa. Haya yote yalifanyika kwa musaada wa mufalme Kiro wa Persia.