Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ezra 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya mambo haya yote kutendeka, viongozi wakanifikia na kunipa habari hii: “Watu wa Israeli, makuhani na Walawi hawakujitenga na wakaaji wa inchi ambao wanatenda machukizo: Waamoni, Wamoabu na Wamisri, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wayebusi na Waamori.

Gade chapit la Kopi




Ezra 9:1
37 Referans Kwoze  

Wakati ule, walikuwa wamejitenga mbali na watu wa mataifa mengine, wakasimama na kuungama zambi zao na maovu ya babu zao.


Maana namna gani itajulikana kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee kati ya watu wote katika dunia.


Basi wakubwa na watu wote wakawaambia makuhani na manabii: Mutu huyu hastahili hukumu ya kifo. Amesema nasi kwa jina la Yawe, Mungu wetu.


Basi, wakubwa wa Yuda waliposikia mambo hayo, wakapanda kutoka kwa nyumba ya mufalme, wakaenda kwenye nyumba ya Yawe, wakaikaa kwenye mulango ulioitwa: “Mulango Mupya”.


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Lakini walichanganyika na watu wa mataifa, wakajifunza kutenda mambo yao.


Halafu tukamwomba Mungu wetu na kuweka ulinzi juu yao, muchana na usiku.


Ikiwa mutu yeyote atashindwa kufika katika muda wa siku tatu, kulingana na amri iliyotolewa na viongozi, mali yake yote itanyanganywa, naye mwenyewe atatengwa mbali na makutano na jamii ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho.


Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kuiga mienendo miovu ya mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake wa Israeli walipokuwa wanaingia.


Solomono alipenda sana wanawake wa kigeni: binti ya mufalme wa Misri, wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni, na Wahiti,


“Mutakapofika katika ile inchi Yawe, Mungu wenu, anayowapa, musifuate zile tabia za kuchukiza za mataifa ya huko.


Kutoka vilele vya mawe makubwa ninawaona, kutoka juu ya milima nawachungulia, hilo taifa linalokaa peke yake, lisilojiona kuwa sawa na mataifa mengine.


Musifanye kama vile watu wa inchi ya Misri ambako mulikaa wanavyofanya, wala musifanye kama vile watu wa inchi ya Kanana ambako ninawapeleka wanavyofanya. Musifuate desturi zao hata kidogo.


Malaika wangu atakapowaongoza na kuwafikisha katika inchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanana, Wahivi na Wayebusi, nami nitawaangamiza wale wote.


Na wakati Yawe atakapowafikisha katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Wahivi, na Wayebusi, inchi ambayo aliwaapia babu zenu kwamba atawapa ninyi, inchi inayotiririka maziwa na asali, munapaswa kushika sikukuu hii kila mwaka katika mwezi huu wa kwanza.


Wazao wako watarudi hapa katika kizazi cha ine, kwa sababu uovu wa Waamori haujakamilika bado.”


Hivyo, kwenye sehemu za chini za ukuta ambazo zilikuwa bado kumalizika, nyuma ya ukuta, katika pahali pa wazi, nikawapanga watu kulingana na jamaa zao wakiwa na mapanga, mikuki na pinde.


Tena wakati ule nikaona Wayuda waliooa wanawake toka Asidodi, Amoni na Moabu;


Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na katika Yerusalema. Wamechafua hekalu la Yawe analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni.


Wakati huohuo mutu mumoja akamuleta mwanamuke mumoja Mumidiani katika nyumba yake, Musa na Waisraeli wote pamoja wakiwa wanaomboleza kwenye mulango wa hema la mukutano.


“Yawe, Mungu wenu atawafikisha kwenye inchi ambayo mutakwenda kufanya makao yenu na atafukuza mataifa mengi kutoka inchi hiyo. Mutakapoingia, atafukuza mbele yenu mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi: Wahiti, Wagirgasi, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.


“Musiwachukie Waedomu; hao ni wandugu zenu. Na musiwachukie Wamisri, maana mulikaa katika inchi yao kama vile wageni.


Maana, kama mukimwasi Yawe na kujiunga na mataifa haya yaliyobaki kati yenu, mukioa kwao nao wakioa kwenu,


Watu wengine wote waliobaki kati ya Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, ni kusema wote ambao hawakukuwa Waisraeli,


Halafu Sekania mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Elamu, akamwambia Ezra: “Tumekosa uaminifu kwa Mungu kwa kuoa wanawake wa kigeni wa inchi hii, lakini hata hivyo bado kuna tumaini kwa ajili ya Israeli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite