Ezra 7:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20028 Wakafika Yerusalema katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Artasasta. Gade chapit la |
Katika siku hizo tatu, kwa siku ya makumi mbili ya mwezi wa tisa, watu wote walioishi katika majimbo ya Yuda na Benjamina wakafika Yerusalema na kukusanyika katika kiwanja cha nyumba ya Mungu. Watu wote walikuwa wakitetemeka kwa sababu ya shauri waliloitiwa na kwa ajili ya mvua nyingi iliyokuwa ikinyesha.
Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.