Ezra 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20023 “Katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mufalme Kiro alitoa amri kwamba nyumba ya Mungu ijengwe upya katika Yerusalema, na ikuwe pahali pa kutolea sadaka na sadaka za kuteketezwa kwa moto. Urefu wake kwenda juu utakuwa metre makumi mbili na saba na upana wake metre makumi mbili na saba. Gade chapit la |
Basi, sasa unitumie mutu mwenye ujuzi wa kutengeneza vyombo kwa zahabu, feza, shaba, na chuma, na nguo ya rangi nyekundu-nyeusi, za rangi nyekundu na ya samawi, anayejua vilevile kuchora. Yeye atashirikiana katika kazi hiyo na wafundi wanaokuwa pamoja nami katika Yuda na Yerusalema, ambao baba yangu Daudi aliwaweka.
Watu walitoa feza za kuwalipa waseremala na wajengaji, walitoa vilevile chakula, vinywaji na mafuta, kusudi vipelekwe katika miji ya Tiro na Sidona kubadilishwa na miti ya mierezi kutoka Lebanoni. Miti hiyo ililetwa kwa njia ya bahari mpaka Yopa. Haya yote yalifanyika kwa musaada wa mufalme Kiro wa Persia.
Ninataka kujenga nyumba ya kumwabudia Yawe wangu. Nitaitakasa kwa ajili yake, nayo itakuwa pahali pa kufukiza ubani wenye harufu nzuri mbele yake, na vilevile pahali pa kumutolea mikate mitakatifu siku zote, na sadaka za kuteketezwa asubui na magaribi na za siku za Sabato, za Mwandamo wa Mwezi, na sikukuu zingine za Yawe, Mungu wetu, kama vile alivyoagiza Waisraeli milele.