Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ezra 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kisha Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wenzao, wakakwenda Yerusalema na kuuliza: “Nani aliyewaamuru kuijenga nyumba hii mpaka kuimaliza?”

Gade chapit la Kopi




Ezra 5:3
12 Referans Kwoze  

Halafu Dario akatuma ujumbe huu: Kwa Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wakubwa wenzako katika jimbo. Musiende kule kwenye hekalu,


Basi, Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi, na wakubwa wenzao, wakafanya bidii kwa kutimiza maagizo ya mufalme.


Tuliwauliza viongozi hao watuambie ni nani aliyewapa amri ya kuijenga upya nyumba hii mpaka kuimaliza.


Basi sasa, kila mutu kati yenu ninyi wote munaokuwa watu wake, Mungu wake akuwe naye na aende katika Yerusalema huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yawe, Mungu wa Israeli, Mungu anayeabudiwa kule Yerusalema.


Wakasimamisha Petro na Yoane mbele yao na kuwauliza: “Ni kwa uwezo gani au kwa jina la nani ninyi mumefanya jambo lile?”


Yesu akaingia ndani ya hekalu. Alipokuwa akifundisha, wakubwa wa makuhani pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka yale?”


Mimi mufalme Artasasta, ninatoa amri kwa walinzi wa hazina wote katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati kwamba kitu chochote Ezra atakachohitaji, kuhani na mwandishi wa Sheria ya Mungu wa mbinguni, mutamupa, tena bila kusita,


Basi, Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wenzao, wakamwandikia mufalme Dario.


Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba Wayuda waliokuja hapa kutoka maeneo mengine ya ufalme wako wamekwenda Yerusalema na wanaujenga upya muji huo wa waasi na waovu. Wanamalizia kujenga kuta zake na kutengeneza musingi.


Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Hii barua inatoka kwa mutawala Rehumu na kwa Simusayi, karani wa jimbo pamoja na wenzetu, na waamuzi, wakubwa wote ambao pale mbele walitoka Ereki, Babeli, Susani, Dini, Afarsati, Terpeli, Deha na Elamu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite