Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ezra 4:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lakini Zerubabeli, Yesua na viongozi wengine wa ukoo za Waisraeli wakawaambia: “Sisi hatuhitaji musaada wowote kutoka kwenu kwa kuijenga nyumba ya Mungu wetu. Sisi wenyewe tutamujengea Yawe, Mungu wa Israeli, kama vile mufalme Kiro wa Persia alivyotuamuru.”

Gade chapit la Kopi




Ezra 4:3
16 Referans Kwoze  

Nikawajibu: “Mungu wa mbinguni atatufanikisha katika kazi hii, nasi tunaokuwa watumishi wake tutaanza kujenga. Lakini ninyi hamuna sehemu au haki wala ukumbusho katika Yerusalema.”


Wewe hauna sehemu wala haki yoyote katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mukamilifu mbele ya Mungu.


“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.


Kwa ajili ya mutumishi wangu Yakobo, muchaguliwa wangu Israeli, nimekuita kwa jina lako; nimekupa jina la heshima ingawa wewe haunijui.


Ndimi ninasema juu ya mufalme Kiro: Ni muchungaji niliyemuchagua kwa ajili yangu. Yeye atatimiza mipango yangu yote. Ndimi ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema utajengwa tena upya; na juu ya hekalu: Musingi wako utawekwa tena.


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Kiro mufalme wa Persia, kusudi litimie neno la Yawe alilolisema kwa njia ya nabii Yeremia, Yawe aliamusha nia ya Kiro naye akatoa amri hii katika ufalme wake wote, vilevile alituma habari hizo kwa njia ya maandiko:


Basi yule mwanamuke Musamaria akamwambia Yesu: “Namna gani wewe Muyuda unaweza kuniomba mimi Musamaria maji ya kunywa?” (Wayuda hawakukuwa na ushirika na Wasamaria.)


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Kiro mufalme wa Persia, Yawe akatimiza neno alilosema kwa njia ya nabii Yeremia. Yawe akaamusha nia ya Kiro mufalme wa Persia, naye akatoa amri hii katika ufalme wake, vilevile amri hiyo ikatolewa kwa maandiko:


Hivi ndivyo Kiro mufalme wa Persia anavyosema: Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote katika ulimwengu na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, huko Yuda.


Basi, watu wakaanza kazi katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili nyuma ya kufikia kwenye nyumba ya Mungu katika Yerusalema. Zerubabeli, mwana wa Saltieli, Yesua mwana wa Yosadaki, wandugu zao wengine, makuhani, Walawi na watu wengine wote waliorudi Yerusalema kutoka katika uhamisho, wakajiunga nao katika kazi hiyo. Walawi wote waliokuwa na umri wa miaka makumi mbili au zaidi, walichaguliwa kwa kusimamia kazi ya kuijenga upya nyumba ya Yawe.


Basi sasa, kila mutu kati yenu ninyi wote munaokuwa watu wake, Mungu wake akuwe naye na aende katika Yerusalema huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yawe, Mungu wa Israeli, Mungu anayeabudiwa kule Yerusalema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite