Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ezra 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba Wayuda waliokuja hapa kutoka maeneo mengine ya ufalme wako wamekwenda Yerusalema na wanaujenga upya muji huo wa waasi na waovu. Wanamalizia kujenga kuta zake na kutengeneza musingi.

Gade chapit la Kopi




Ezra 4:12
22 Referans Kwoze  

Tuliwauliza viongozi hao watuambie ni nani aliyewapa amri ya kuijenga upya nyumba hii mpaka kuimaliza.


Kisha Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wenzao, wakakwenda Yerusalema na kuuliza: “Nani aliyewaamuru kuijenga nyumba hii mpaka kuimaliza?”


Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.


Muepuke ubaya wa kila namna.


Tumetambua kwamba mutu huyu ni wa hatari sana, ameanzisha fujo kati ya Wayuda wote katika dunia. Tena yeye ni mukubwa wa chama cha Wanazareti.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Wao wakaniambia: “Wayuda walioponyoka na kubaki katika jimbo lile, wako katika taabu nao wanazarauliwa. Ukuta wa Yerusalema umebomolewa na milango yake imeteketezwa.”


Nimetoa amri uchunguzi ufanyike na imegunduliwa kuwa ni kweli kwamba tangu zamani muji huu wa Yerusalema umekuwa ukiwapinga wafalme na kwamba watu wake wamekuwa waasi na wachochezi wakubwa.


kusudi ufanye uchunguzi katika kitabu cha habari za babu zako. Humo utagundua kwamba tangu zamani, muji huu ulikuwa wa waasi na umewasumbua sana wafalme na watawala wa majimbo, na kuwa tangu zamani watu wake ni wachochezi sana; ndiyo sababu muji huo uliangamizwa.


Nebukadneza mufalme wa Babeli akaishambulia inchi ya Yuda. Yoyakimu akamutumikia kwa miaka mitatu halafu akaacha kumutii, akamwasi.


Unazani kwamba maneno matupu ndiyo maarifa na nguvu katika vita? Ni nani unayemutegemea hata ukaniasi?


Kwa mufalme Artasasta: Sisi watumishi wako katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, tunakutumia salamu.


Basi, Hamani akamwambia mufalme: “Kuna watu wa taifa moja wanaokuwa kila nafasi katika utawala wako, nao wako katika kila jimbo. Watu hao wana sheria zinazokuwa tofauti kabisa na za watu wengine. Vilevile, wao hawazitii sheria zako, kwa hiyo haikufaidii kwa kitu chochote kuwavumilia.


Wakati huo, watu wamoja kati ya Wakaldea wakajitokeza na kuwashitaki Wayuda. Walimwambia mufalme Nebukadneza:


Na barua yenyewe iliandikwa hivi: Kuna habari zilizoenezwa kati ya mataifa jirani, na Gesemi anahakikisha habari hizi, kwamba wewe pamoja na Wayuda wenzako munakusudia kuasi. Hii ndiyo sababu munaujenga upya ukuta. Kulingana na habari hizo, wewe unakusudia kuwa mufalme wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite