Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ezra 4:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kwa mufalme Artasasta: Sisi watumishi wako katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, tunakutumia salamu.

Gade chapit la Kopi




Ezra 4:11
7 Referans Kwoze  

Basi yule mwanamuke Musamaria akamwambia Yesu: “Namna gani wewe Muyuda unaweza kuniomba mimi Musamaria maji ya kunywa?” (Wayuda hawakukuwa na ushirika na Wasamaria.)


pamoja na watu wa mataifa mengine ambao Asurbanipali, mutu mukubwa na mwenye nguvu akawahamisha na kuwaweka katika muji wa Samaria na pahali pengine katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.


Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba Wayuda waliokuja hapa kutoka maeneo mengine ya ufalme wako wamekwenda Yerusalema na wanaujenga upya muji huo wa waasi na waovu. Wanamalizia kujenga kuta zake na kutengeneza musingi.


Basi, Yezebeli akaandika barua kwa jina la Ahabu na kuzipiga muhuri wa mufalme. Kisha akapeleka barua hizo kwa wazee na watu wenye heshima walioishi na Naboti kule katika muji.


Wakaijenga mazabahu hiyo pahali palepale ilipokuwa hapo zamani, kwa kuwa waliwaogopa watu waliokuwa wanaishi katika inchi hiyo. Kisha wakakuwa wanamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake kila siku asubui na magaribi.


Basi, Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wenzao, wakamwandikia mufalme Dario.


Huu ndio mufano wa barua ambayo Artasasta alimupa Ezra, kuhani na mwandishi, na mwenye ujuzi katika amri na masharti ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite