Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Ezekieli 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nilipoangalia niliona upepo wa zoruba unavuma kutokea upande wa kaskazini: kulikuwa wingu kubwa lililozungukwa na mwangaza, na moto ulitokea humo mufululizo na katikati ya huo moto kulikuwa kitu kinachometameta kama shaba.

Gade chapit la Kopi




Ezekieli 1:4
35 Referans Kwoze  

Sehemu ya juu ya mwili wake ilingaa kama shaba, nao ulikuwa sawa unazungukwa na moto pande zote. Tokea sehemu ya chini ya mwili wake, niliona kitu kama moto. Mwangaza ulimuzunguka.


Nilipoangalia, nikaona kitu kilichofanana na mwanadamu. Sehemu yake ya chini, iliyoonekana kama ndio kiuno chake, ilikuwa kama moto. Toka kiuno chake kwenda juu alimetameta kama vile shaba.


Angalia, zoruba kali kutoka kwa Yawe; kasirani yake imeamuka, upepo mukali utapiga kichwa cha mwovu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Hasara italifikia taifa kwa taifa, na zoruba itavuma kutoka miisho ya dunia.


Ujumbe wa Mungu juu ya jangwa kando ya bahari. Kama upepo mukali unaovuma kutoka kusini, washambulizi wanakuja kutokea katika jangwa, kutoka katika inchi ya kutisha.


Miguu yake ilingaa kama shaba iliyosafishwa vizuri sana katika furu ya moto, na sauti yake ilinguruma kama maporomoko ya maji mengi.


kwa maana Mungu wetu ni kama moto wenye kuteketeza.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.


Muinue bendera ya vita kuelekea Sayuni, kusudi mukimbie, wala musisitesite! Yawe analeta hasara, analeta maangamizi makubwa kutoka kaskazini.


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.


Mungu wetu anakuja, lakini si kimyakimya: moto wenye kuteketeza unamutangulia, na zoruba kali inamuzunguka.


Waimbaji na wapiga baragumu wote pamoja walitoa sauti kwa pamoja na matoazi na vyombo vingine vya muziki, wakimusifu Yawe wakiimba: “Yeye ni muzuri. Wema wake unadumu milele.” Wakati ule nyumba ya Yawe ikajazwa na wingu.


Yawe akamwambia: “Kwenda usimame juu ya mulima, mbele yangu mimi Yawe.” Basi, Yawe akapita na kuuvumisha upepo mukali ambao uliporomosha milima na kuvunja mawe makubwa. Lakini Yawe hakukuwa katika upepo ule. Upepo ukapita, kukakuwa tetemeko la inchi. Lakini Yawe hakukuwa katika tetemeko la inchi.


Sasa uwaambie hao manabii wanaopakaa chokaa ukuta huo kwamba kutanyesha mvua kubwa ya mawe na zoruba itavuma na ukuta huo utaanguka.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema: Kwa kasirani yangu nitazusha upepo wa zoruba na mvua nyingi ya mawe, navyo vitauangusha ukuta huo.


Maono hayo yalikuwa kama maono niliyoyaona wakati Mungu alipokuja kuuangamiza Yerusalema. Vilevile yalifanana na maono niliyoyaona karibu na muto Kebari. Nikaanguka uso mpaka chini.


Lile gari linalokokotwa na farasi weusi linakwenda upande wa kaskazini, lile linalokokotwa na farasi weupe linakwenda upande wa magaribi, na lile linalokokotwa na farasi wa kijivujivu linakwenda upande wa kusini.


mvua kubwa ya mawe iliyofuatana na mufululizo wa umeme, ambayo hakuna mwanainchi yeyote wa Misri aliyepata hata kidogo kushuhudia mbele.


Walipokuwa wanatembea na kuongea, kwa rafla gari la moto lililokokotwa na farasi wa moto likawatenganisha. Naye Elia akanyanyuliwa mbinguni katika upepo wa kuzungukazunguka.


Halafu Yawe akamujibu Yobu kutoka katika zoruba:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite