Ezekieli 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Juu ya nyuso zao: kila kimoja kilikuwa na uso wa mutu upande wa mbele, uso wa simba upande wa kuume, uso wa ngombe upande wa kushoto, na uso wa tai upande wa nyuma.
Kila kerubi alikuwa na nyuso ine: uso wa kwanza ulikuwa wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa ine ulikuwa wa tai.
Kiumbe cha kwanza kilifanana na simba, kiumbe cha pili kilifanana na mwana-ngombe na kiumbe cha tatu kilifanana na mutu na kiumbe cha ine kilifanana na tai anayeruka.
Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”
Nyama wa kwanza alikuwa kama simba, na alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikiwa ninamwangalia, mabawa yake yaliongolewa, naye akainuliwa na kusimama kwa miguu miwili kama mutu. Kisha, akapewa akili ya kimutu.
Siku hiyo ya saba, mbele ya jua kutua, wakamwambia Samusoni, “Ni kitu gani kitamu kuliko asali? Ni nani mwenye nguvu kuliko simba?” Samusoni akawajibu: “Kama hamungejishugulisha na mwana-ngombe wangu hamungeweza kukitegua kitendawili changu.”
Kwa upande wa magaribi, wale wanaokuwa chini ya bendera ya kundi la Efuraimu watapiga kambi kulingana na jeshi lake kiongozi wao akiwa Elisama mwana wa Amihudi,
Wale watakaopiga kambi upande wa mashariki watakuwa kikundi cha watu wanaokuwa chini ya bendera ya Yuda na kiongozi wao atakuwa Nasoni mwana wa Aminadabu.
Wandugu zangu, musikuwe kama watoto kwa kufikiri: lakini katika mambo mabaya, iwatokee kutenda kama watoto wachanga. Inafaa mafikiri yenu yakuwe kama ya watu wazima.
uso wa mwanadamu ulioelekea kwenye muti wa ngazi upande mumoja na uso wa simba ulioelekea kwenye muti wa ngazi upande mwingine. Hivi ndivyo ilivyokuwa kwenye nyumba nzima,