Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 9:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.

Gade chapit la Kopi




Esteri 9:25
19 Referans Kwoze  

Anachimba shimo, na kulirefusha, kisha anatumbukia humo yeye mwenyewe.


Anayeanguka juu ya jiwe hili atavunjikavunjika, na yule litakayemwangukia, atapondekana.]”


Waovu wanaswe katika mitego yao wenyewe, wakati mimi ninaponyoka.


Ee Yawe, usiwape waovu vitu wanavyotaka, wala mipango yao mibaya usiifanikishe.


Hapo mufalme Ahasuero akamwuliza malkia Esteri: “Ni nani huyo anayesubutu kufanya jambo kama hilo? Yuko wapi mutu huyo?”


Tena alipogundua kwamba Mordekayi alikuwa Muyuda, akaamua kwamba kumwazibu peke yake haitoshi. Basi akafanya shauri la kuwaangamiza Wayuda wote, watu wa ukoo wa Mordekayi, katika utawala wa mufalme Ahasuero.


Maana, mimi na watu wangu tumeuzishwa kusudi tuuawe, tuangamizwe na kuteketezwa kabisa. Kama tungeuzishwa tu kuwa watumwa na wajakazi, ningekaa kimya wala nisingekusumbua. Ingawa tutateswa hakuna adui atakayeweza kulipa hasara hii kwa mufalme.”


Ee Yawe, Bwana wangu, mukombozi wangu mukubwa, umenikinga salama wakati wa vita.


Lakini siku moja, –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi– ule musumari uliopigiliwa pahali pagumu utaregea kwa uzito. Utakatwa na kuanguka. Yawe amesema.


Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.


tafazali wewe usikilize kutokea kule mbinguni, utende na kuwahukumu watumishi wako. Anayekuwa na kosa umwazibu kwa kadiri ya makosa yake; asiyekuwa na kosa umwachilie na kumupatia haki kwa kadiri ya haki yake.


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Uharibifu wake utamurudilia yeye mwenyewe; ukali wake utamwangukia yeye mwenyewe.


Atawarudishia uovu wao wenyewe, atawateketeza kwa sababu ya ubaya wao. Yawe, Mungu wetu, atawateketeza kabisa!


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Anayechimbia mwenzake shimo, anatumbukia ndani mwenyewe; anayewaporomoshea wengine jiwe, litamurudilia mwenyewe.


Siku inakaribia ambapo mimi Yawe nitayahukumu mataifa yote. Kama vile mulivyowatendea wengine, ndivyo mutakavyotendewa, mutalipwa kulingana na matendo yenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite