Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 9:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari, Wayuda wakakusanyika tena, wakawaua watu mia tatu zaidi katika muji wa Susani. Lakini hawakunyanganya mali za watu.

Gade chapit la Kopi




Esteri 9:15
10 Referans Kwoze  

wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedata, adui ya Wayuda. Hata hivyo, hawakunyanganya mali zao.


Kwa njia ya barua hizi mufalme akawaruhusu Wayuda katika kila muji kukusanyika kwa kuyalinda maisha yao. Walikuwa na ruhusa ya kuharibu, kuua bila huruma na kuangamiza kundi lolote la watu au jimbo, lenye kuwashambulia kwa silaha pamoja na wanawake na watoto wao, na kunyanganya mali zao.


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Muepuke ubaya wa kila namna.


Wayuda waliokuwa katika majimbo nao vilevile wakajitayarisha kuyalinda maisha yao. Wakaokolewa kutoka kwa waadui zao, wakawaua watu yapata elfu kumi na tano, lakini hawakunyanganya mali zao.


Esteri akasema: “Ikikupendeza, ewe mufalme, kesho uwaruhusu Wayuda wanaokuwa Susani wafanye kama agizo la leo lilivyokuwa. Tena, uamuru wana kumi wa Hamani watundikwe kwenye miti.”


Katika kila muji wa kila jimbo wa mufalme Ahasuero, Wayuda walijitayarisha vizuri kumushambulia mutu yeyote ambaye angejaribu kuwazuru.


Halafu mufalme akamwambia malkia Esteri: “Katika muji mukubwa peke yake Wayuda wamewaua watu mia tano, pamoja na wana kumi wa Hamani. Unafikiri wamefanya nini kule katika majimbo! Unataka nini sasa? Maana utatimiziwa. Uniambie, unataka nini zaidi, nawe utapewa.”


Mufalme akaamuru hayo yatimizwe, na tangazo likatolewa katika muji Susani. Wana kumi wa Hamani wakatundikwa juu ya muti.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite