Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 9:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mufalme akaamuru hayo yatimizwe, na tangazo likatolewa katika muji Susani. Wana kumi wa Hamani wakatundikwa juu ya muti.

Gade chapit la Kopi




Esteri 9:14
9 Referans Kwoze  

Esteri akasema: “Ikikupendeza, ewe mufalme, kesho uwaruhusu Wayuda wanaokuwa Susani wafanye kama agizo la leo lilivyokuwa. Tena, uamuru wana kumi wa Hamani watundikwe kwenye miti.”


Siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari, Wayuda wakakusanyika tena, wakawaua watu mia tatu zaidi katika muji wa Susani. Lakini hawakunyanganya mali za watu.


Kisha Balamu akawaangalia Waamaleki, akatoa mashairi haya: Amaleki ni taifa lenye nguvu kuliko yote, lakini kwa mwisho litaangamia kabisa.


Ninaamuru kwamba katika utawala wangu, Mwisraeli yeyote, au kuhani wao, au Mulawi, akitaka kurudi Yerusalema kwa mapenzi yake, anaweza kwenda pamoja nawe.


Harbona, mumoja wa wale matowashi waliomutumikia mufalme, akasema: “Hamani amesubutu hata kutengeneza muti wa kumutundikia Mordekayi ambaye aliyaokoa maisha yako, ewe mufalme. Muti huo, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili, bado uko kule katika nyumba yake.” Hapo mufalme akaamuru: “Mumutundike Hamani juu ya muti uleule.”


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Waovu wanaangamizwa na kutoweka kabisa, lakini jamaa ya wenye haki itasimama.


Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite