Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Esteri 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ni kusema mwezi wa Adari, ilipofika, siku ambayo tangazo la mufalme lingetimizwa, na waadui za Wayuda walitarajia kuwashinda Wayuda, ikageuzwa kuwa siku ya ushindi kwa Wayuda juu ya waadui zao.

Gade chapit la Kopi




Esteri 9:1
13 Referans Kwoze  

Jambo hili lingefanyika katika majimbo yote ya mufalme Ahasuero, katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ni kusema Adari.


Wajumbe wakazipeleka barua hizo kwa kila jimbo katika utawala ule. Tangazo hilo lilisema kwamba kwa siku moja tu, ni kusema siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari, Wayuda wote – tangia kwa vijana mpaka wazee, wanawake na watoto, wote wauawe, waangamizwe na kuteketezwa kabisa, na mali zao zote zinyanganywe.


Watu wa mataifa mengine walikasirika, lakini kasirani yako imetokea. Sasa ni wakati wa kuhukumu waliokufa, nao wakati wa kuwapa waliokutumikia zawadi, ndio manabii wako, na wote wanaoheshimu jina lako, wakubwa na wadogo. Ni wakati wa kuangamiza wale wanaoharibu dunia!”


Usikie, ee Yawe, unihurumie; ee Yawe, unisaidie!”


Petro alipotambua kwamba mambo yaliyotokea ni ya kweli akasema: “Sasa ninajua hakika kwamba Bwana alimutuma malaika wake kuniokoa katika mikono ya Herode na katika mabaya yote Wayuda waliotaka kunitendea.”


Siku hiyo ilikuwa ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari. Siku iliyofuata ya kumi na ine, wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na sherehe.


Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa mufalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza unaoitwa Nisani, wakapiga Purimu, maana yake kura, mbele ya Hamani kusudi ajue mwezi na siku ya kuwaangamiza. Basi kura ikaangukia mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari.


Uliwakimbiza waadui zangu, na wale walionichukia niliwaangamiza.


Yawe atawatetea watu wake, na kuwahurumia watumishi wake, wakati atakapoona nguvu zao zimeisha wala hakuna aliyebaki, mufungwa au mutu huru.


Maana, ninaweza namna gani kuvumilia kuona watu wangu wanaangamizwa na wandugu zangu wanauawa?”


Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita; uliwaporomosha waadui chini yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite